Zaburi 64:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Na watu wote wataogopa, Wataitangaza kazi ya Mungu, Na kuyafahamu matendo yake. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Hapo watu wote wataogopa; watatangaza aliyotenda Mungu, na kufikiri juu ya matendo yake. Biblia Habari Njema - BHND Hapo watu wote wataogopa; watatangaza aliyotenda Mungu, na kufikiri juu ya matendo yake. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Hapo watu wote wataogopa; watatangaza aliyotenda Mungu, na kufikiri juu ya matendo yake. Neno: Bibilia Takatifu Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda. Neno: Maandiko Matakatifu Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda. BIBLIA KISWAHILI Na watu wote wataogopa, Wataitangaza kazi ya Mungu, Na kuyafahamu matendo yake. |
Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumainia BWANA.
Hapo waliingiwa na hofu pasipokuwapo hofu, Maana Mungu ameitawanya mifupa yake aliyekuhusuru. Umewatia aibu, Kwa sababu MUNGU amewadharau.
Na mwanadamu atasema, Hakika iko thawabu yake mwenye haki. Hakika yuko Mungu Anayehukumu katika dunia.
Uwakomeshe kwa hasira, Uwakomeshe watoweke, Wajue ya kuwa Mungu atawala katika Yakobo, Na hata miisho ya dunia.
Na kinubi, na zeze, na matari, na filimbi, na mvinyo, zote ziko katika karamu zao; lakini hawaiangalii kazi ya BWANA wala kuyafikiri matendo ya mikono yake.
Sauti yao wakimbiao na kuokoka, Kutoka katika nchi ya Babeli, Ili kutangaza katika Sayuni kisasi cha BWANA, Mungu wetu, Kisasi cha hekalu lake.
BWANA ameitokeza haki yetu; Njooni, tutangaze katika Sayuni Habari za kazi ya BWANA, Mungu wetu.
Nao watawafariji ninyi, mtakapoona njia yao na matendo yao; nanyi mtajua ya kuwa sikufanya bila sababu mambo yote niliyoutenda, asema Bwana MUNGU.
Ni nani aliye na hekima, naye atayafahamu mambo haya? Ni nani aliye na busara, naye atayajua? Kwa maana njia za BWANA zimenyoka, nao wenye haki watakwenda katika njia hizo; bali waasio wataanguka ndani yake.
Na katika saa ile palikuwa na tetemeko kuu la nchi, na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka; wanadamu elfu saba wakauawa katika tetemeko lile. Na waliobakia wakaingiwa na hofu, wakamtukuza Mungu wa mbingu.