Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 62:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Hadi lini mtamshambulia mtu, Mpate kumwua ninyi nyote pamoja? Kama ukuta unaoinama, Kama ua ulio tayari kuanguka,

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hata lini mtanishambulia mimi? Hata lini nyinyi nyote mtanipiga, mimi niliye kama kiambaza kilichoinama, kama ukuta unaoanza kubomoka?

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hata lini mtanishambulia mimi? Hata lini nyinyi nyote mtanipiga, mimi niliye kama kiambaza kilichoinama, kama ukuta unaoanza kubomoka?

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hata lini mtanishambulia mimi? Hata lini nyinyi nyote mtanipiga, mimi niliye kama kiambaza kilichoinama, kama ukuta unaoanza kubomoka?

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mtanishambulia hadi lini? Je, ninyi nyote mtanitupa chini: Mimi niliye kama ukuta ulioinama, kama uzio unaotikisika?

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mtamshambulia mtu hata lini? Je, ninyi nyote mtamtupa chini, ukuta huu ulioinama na uzio huu unaotikisika?

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Hadi lini mtamshambulia mtu, Mpate kumwua ninyi nyote pamoja? Kama ukuta unaoinama, Kama ua ulio tayari kuanguka,

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 62:3
19 Marejeleo ya Msalaba  

Wamtumainio BWANA ni kama mlima Sayuni, Ambao hautikisiki, wakaa milele.


Waliowaza mabaya mioyoni mwao, Kila siku huchochea vita.


Nimemweka BWANA mbele yangu daima, Kwa kuwa yuko kuliani mwangu, sitaondoshwa.


Namwita BWANA astahiliye kusifiwa, Hivyo nitaokoka na adui zangu.


Wakipanga kukutenda mabaya, Kwa miango ya hila, hawatafanikiwa.


Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego; Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya; Na kufikiri hila mchana kutwa.


Enyi wanadamu, hadi lini utukufu wangu utafedheheka? Je! Mtapenda ubatili na kutafuta uongo hadi lini?


Hadi lini mtahukumu kwa dhuluma, Na kuzikubali nyuso za wabaya?


Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao, na kumwambia, BWANA, Mungu wa Waebrania, asema hivi, Je! Utakataa hata lini kujinyenyekeza mbele zangu? Wape watu wangu ruhusa waende zao, ili wanitumikie.


BWANA akamwambia Musa, Mtakataa kuyashika maagizo yangu na sheria zangu hata lini?


Enyi wajinga, hata lini mtapenda ujinga? Na wenye dharau kupenda dharau yao, Na wapumbavu kuchukia maarifa?


Ewe mvivu, utalala hadi lini? Utaondoka lini katika usingizi wako?


Ee Yerusalemu, jioshe moyo wako usiwe na uovu, upate kuokoka. Mawazo yako mabaya yatakaa ndani yako hata lini?


Ingawa nimewafundisha na kuwatia nguvu mikono yao, hata hivyo hukusudia udhalimu juu yangu.


Yesu akajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hadi lini? Nitachukuliana nanyi hadi lini? Mleteni huku kwangu.


Wayahudi nao wakamshitaki, wakisema ya kuwa ndivyo yalivyo.


Daudi akasema, Aishivyo BWANA, BWANA atampiga; au siku yake ya kufa itampata; atashuka kwenda vitani na kupotea.