Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 6:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

BWANA, unifadhili, maana ninanyauka; BWANA, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Unihurumie, ee Mwenyezi-Mungu, nimeishiwa nguvu; uniponye, ee Mwenyezi-Mungu, nataabika mpaka mifupani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Unihurumie, ee Mwenyezi-Mungu, nimeishiwa nguvu; uniponye, ee Mwenyezi-Mungu, nataabika mpaka mifupani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Unihurumie, ee Mwenyezi-Mungu, nimeishiwa nguvu; uniponye, ee Mwenyezi-Mungu, nataabika mpaka mifupani.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Unirehemu Mwenyezi Mungu, kwa maana nimedhoofika; Ee Mwenyezi Mungu, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Unirehemu bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

BWANA, unifadhili, maana ninanyauka; BWANA, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 6:2
21 Marejeleo ya Msalaba  

Abrahamu akamwomba Mungu, Mungu akamponya Abimeleki, na mkewe, na wajakazi wake, nao wakazaa wana.


Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.


Kwani yeye huumiza, lakini tena huuguza; Yeye hutia jeraha, na mikono yake huponya.


Nimemwagika kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na kuyeyuka ndani ya moyo wangu.


Ee BWANA, Mungu wangu, Nilikulilia ukaniponya.


Maana maisha yangu yamekwisha kwa huzuni, Na miaka yangu kwa maumivu. Nguvu zangu zimeniishia kwa uovu wangu, Na mifupa yangu imepooza.


Nilipokosa kuungama dhambi zangu, mifupa yangu ilipooza Kwa kulia kwangu mchana kutwa.


Kwa maana mishale yako imenichoma, Na mkono wako umenipata.


Hamna uzima katika mwili wangu Kwa sababu ya ghadhabu yako. Wala hamna amani mifupani mwangu Kwa sababu ya hatia zangu.


Maana viuno vyangu vimejaa homa, Wala hamna uzima katika mwili wangu.


Unifanye kusikia furaha na shangwe, Mifupa uliyoiponda ifurahi.


akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya BWANA, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yoyote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa Mimi ndimi BWANA nikuponyaye.


Ee BWANA, unirudi kwa haki; si kwa hasira yako, usije ukaniangamiza.


Uniponye, Ee BWANA, nami nitaponyeka; uniokoe, nami nitaokoka; kwa maana wewe ndiwe uliye sifa zangu.


Njooni, tumrudie BWANA; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga majeraha yetu.


Musa akamlilia BWANA, akasema, Mponye, Ee Mungu, nakusihi sana.


Na habari zake zikaenea katika Shamu yote; wakamletea wote waliokuwa wagonjwa, walioshikwa na maradhi mbalimbali na mateso, wenye pepo, na wenye kifafa, na wenye kupooza; akawaponya.


Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam, Mimi ndiye, Wala hapana Mungu mwingine ila Mimi; Naua Mimi, nahuisha Mimi, Nimejeruhi, tena naponya; Wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu,