Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 59:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nitakungoja, ewe uliye nguvu yangu; maana wewe, ee Mungu, u ngome yangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nitakungoja, ewe uliye nguvu yangu; maana wewe, ee Mungu, u ngome yangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nitakungoja, ewe uliye nguvu yangu; maana wewe, ee Mungu, u ngome yangu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 59:9
18 Marejeleo ya Msalaba  

Yeye aketiye mbinguni anacheka, Bwana anawafanyia dhihaka.


BWANA akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.


BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? BWANA ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?


Umtumainie BWANA, uwe imara, Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.


Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.


BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.


Ee nguvu zangu, nitakuimbia sifa, Maana Ewe Mungu ndiwe ngome yangu, Mungu wa fadhili zangu.


Mara moja amenena Mungu; Mara mbili nimeyasikia haya, Ya kuwa nguvu zina Mungu,


Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika.


BWANA atakuwa ngome kwake aliyeonewa, Naam, ngome kwa nyakati za shida.


Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana BWANA YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu.


bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watakimbia, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.


ndipo utakapojifurahisha katika BWANA; nami nitakupandisha mahali pa nchi palipoinuka; nitakulisha urithi wa Yakobo baba yako; kwa maana kinywa cha BWANA kimenena hayo.


MUNGU, aliye BWANA, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka.


Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]