Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 57:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Utukuzwe, ee Mungu, juu ya mbingu! Utukufu wako uenee duniani kote!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Utukuzwe, ee Mungu, juu ya mbingu! Utukufu wako uenee duniani kote!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Utukuzwe, ee Mungu, juu ya mbingu! Utukufu wako uenee duniani kote!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 57:5
21 Marejeleo ya Msalaba  

Kisha mfalme Daudi akawaambia kusanyiko lote, Sulemani mwanangu, ambaye Mungu amemchagua peke yake, angali ni mchanga bado na hana uzoefu, nayo kazi hii ni kubwa; kwani nyumba hii ya enzi si kwa mwanadamu, ila kwa BWANA, Mungu.


Na walisifu jina la BWANA, Maana jina lake peke yake limetukuka; Adhama yake i juu ya nchi na mbingu.


Ee BWANA, utukuzwe kwa nguvu zako, Nasi tutaimba na kuuhimidi uwezo wako.


Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.


Na Wewe, BWANA, utawacheka, Utawadhihaki mataifa yote.


Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, Kwa ghafla humpiga bila kuogopa.


Jina lake tukufu na lihimidiwe milele; Dunia yote na ijae utukufu wake. Amina na Amina.


Ee, MUNGU, Bwana wetu Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani kote! Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;


Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.


Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga; Na vigego vyao ni kama visu. Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu.


Na katika siku hiyo mtasema, Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake; Yatangazeni matendo yake kati ya mataifa, Litangazeni jina lake kuwa limetukuka.


Macho ya mwanadamu yaliyoinuka yatashushwa chini, na kiburi cha mwanadamu kitainamishwa, naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.


Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.


Basi sasa, BWANA, Mungu wetu, utuokoe kutoka kwa mkono wake, falme zote za dunia zipate kujua ya kuwa wewe ndiwe BWANA, wewe peke yako.


Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni BWANA wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake.


Kwa maana dunia itajazwa maarifa ya utukufu wa BWANA, kama maji yaifunikavyo bahari.


Mungu alikuja kutoka Temani, Yeye aliye mtakatifu kutoka mlima Parani. Utukufu wake ukazifunika mbingu, Nayo dunia ikajaa sifa yake.


lakini hakika yangu, kama niishivyo, tena kama dunia hii nzima itakavyojawa na utukufu wa BWANA;