Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 49:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Naam, ataliona, hata wenye hekima hufa; Mpumbavu na mjinga hupotea pamoja, Na kuwaachia wengine mali zao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Yeye afahamu kuwa hata wenye hekima hufa, wapumbavu hali kadhalika na watu wajinga. Wote hao huwaachia wengine mali zao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Yeye afahamu kuwa hata wenye hekima hufa, wapumbavu hali kadhalika na watu wajinga. Wote hao huwaachia wengine mali zao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Yeye afahamu kuwa hata wenye hekima hufa, wapumbavu hali kadhalika na watu wajinga. Wote hao huwaachia wengine mali zao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa; wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia na kuwaachia wengine mali yao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa; wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia na kuwaachia wengine mali zao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Naam, ataliona, hata wenye hekima hufa; Mpumbavu na mjinga hupotea pamoja, Na kuwaachia wengine mali zao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 49:10
21 Marejeleo ya Msalaba  

Ee BWANA, kwa mkono wako uniokoe na watu, Watu wa dunia hii ambao fungu lao liko katika maisha haya. Matumbo yao wayajaza kwa hazina yako, Hushiba wana, huwaachia watoto wao akiba zao,


Kweli, watu wote hupita kama kivuli; Wao hujisumbua bure tu; Wanajirundikia mali wala hawajui ni nani atakayeirithi.


Maana atakapokufa hatachukua chochote; Utukufu wake hautashuka ukimfuata.


Nilikuwa kama mjinga, sijui neno; Nilikuwa kama mnyama tu mbele zako.


Bwana, ziko wapi fadhili zako za kwanza, Ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako?


Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini; Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?


Mali hazifaidii kitu siku ya ghadhabu; Bali haki huokoa na mauti.


Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.


Taji la wenye hekima ni mali zao; Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.


Hakika nimekuwa kama mnyama, wala si mtu; Wala sina ufahamu wa mwanadamu;


Kwa sababu Mungu humpa yeye aliyemridhia hekima na maarifa na furaha; bali mkosaji humpa taabu, ili kukusanya na kututa, apate kumpa huyo ambaye Mungu amridhia. Hayo nayo ni ubatili na kufukuza upepo.


Lakini wote pia huwa kama wanyama, ni wapumbavu. Haya ni maelezo ya sanamu, ni shina la mti tu.


Kama kware akusanyaye makinda asiyoyaangua, ndivyo alivyo mtu ajipatiaye mali, wala si kwa haki, katikati ya maisha yake itamtoka, na mwisho wake atakuwa mpumbavu.


Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?


Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu;