Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 48:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Maana, tazama, wafalme walikusanyika; Walikuja wote pamoja.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wafalme walikusanyika, wakaenda pamoja kushambulia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wafalme walikusanyika, wakaenda pamoja kushambulia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wafalme walikusanyika, wakaenda pamoja kushambulia.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maana, tazama, wafalme walikusanyika; Walikuja wote pamoja.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 48:4
12 Marejeleo ya Msalaba  

Basi mfalme wa Shamu moyo wake ukamfadhaika sana kwa ajili ya jambo hili; akawaita watumishi wake, akawaambia, Je! Hamtanionesha, ni mtu yupi miongoni mwenu aliye upande wa mfalme wa Israeli?


Maana asema, Je! Wakuu wangu si wote wafalme?


Wajumbe wa taifa hilo waletewe jibu gani? Ya kuwa BWANA ameiweka misingi ya Sayuni, na ndani yake wale walioonewa katika watu wake watapata kimbilio kwake.


Siku ile wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda; Sisi tunao mji ulio na nguvu; Ataamuru wokovu kuwa kuta na maboma.


Hata ikawa katika siku za Ahazi, mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, mfalme wa Yuda, Resini, mfalme wa Shamu, na Peka, mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli, wakapanda wakaenda Yerusalemu ili kupigana nao, lakini hawakuweza kuushinda.


Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao hao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wakiwa hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;