Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 47:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ametuchagulia urithi wetu, Fahari ya Yakobo ampendaye.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ametuchagulia nchi hii iwe urithi wetu, ambayo ni fahari ya Yakobo anayempenda.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ametuchagulia nchi hii iwe urithi wetu, ambayo ni fahari ya Yakobo anayempenda.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ametuchagulia nchi hii iwe urithi wetu, ambayo ni fahari ya Yakobo anayempenda.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Alituchagulia urithi wetu, fahari ya Yakobo, aliyempenda.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Alituchagulia urithi wetu, fahari ya Yakobo, aliyempenda.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ametuchagulia urithi wetu, Fahari ya Yakobo ampendaye.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 47:4
19 Marejeleo ya Msalaba  

Urithi wa Israeli mtumishi wake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.


Nao watakatifu waliopo duniani, ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.


Na kwa kuwa umeachwa na kuchukiwa, Hata ikawa hapana mtu aliyepita ndani yako, Nitakufanya kuwa fahari ya milele, Furaha ya vizazi vingi.


Lakini mimi nilisema, Nitawezaje kukuweka pamoja na watoto, na kukupa nchi ipendezayo, urithi ulio mwema wa mataifa? Nami nikasema, Mtaniita, Baba yangu, wala hamtageuka na kuacha kunifuata.


katika siku ile niliwainulia mkono wangu, kuwatoa katika nchi ya Misri, na kuwaingiza katika nchi niliyowapelelezea, itiririkayo maziwa na asali, ambayo ni utukufu wa nchi zote;


Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha.


Bwana MUNGU ameapa kwa nafsi yake, asema BWANA, Mungu wa majeshi; Naizira fahari ya Yakobo, nachukizwa na majumba yake; kwa sababu hiyo nitautoa huo mji, pamoja na wote waliomo ndani yake.


BWANA ameapa kwa fahari ya Yakobo, Hakika sitazisahau kamwe kazi zao hata mojawapo.


Kwa maana BWANA anairudisha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli; maana watekao nyara wamewateka, na kuyaharibu matawi ya mizabibu yao.


Nimewapenda ninyi, asema BWANA. Lakini ninyi mwasema, Umetupendaje? Je! Esau siye ndugu yake Yakobo? Asema BWANA; ila nimempenda Yakobo;


Kisha Mfalme atawaambia wale walioko katika mkono wake wa kulia, Njooni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;


macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo;


nayo ni nchi itunzwayo na BWANA, Mungu wako; macho ya BWANA Mungu wako, ya juu yake, tangu mwanzo wa mwaka hadi mwisho wa mwaka.


Hakika awapenda hayo makabila ya watu; Watakatifu wake wote wamo mkononi mwako; Nao waliketi miguuni pako; Watapokea kila mmoja katika maneno yako.


tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu.