Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 47:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kwa kuwa BWANA Aliye Juu, mwenye kuogofya, Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Maana Mwenyezi-Mungu, Mungu Mkuu, anatisha. Yeye ni Mfalme mkuu wa ulimwengu wote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Maana Mwenyezi-Mungu, Mungu Mkuu, anatisha. Yeye ni Mfalme mkuu wa ulimwengu wote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Maana Mwenyezi-Mungu, Mungu Mkuu, anatisha. Yeye ni Mfalme mkuu wa ulimwengu wote.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Jinsi gani alivyo wa kutisha, Mwenyezi Mungu Aliye Juu Sana, Mfalme mkuu juu ya dunia yote!

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Jinsi gani alivyo wa kutisha, bwana Aliye Juu Sana, Mfalme mkuu juu ya dunia yote!

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa kuwa BWANA Aliye Juu, mwenye kuogofya, Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 47:2
18 Marejeleo ya Msalaba  

nikasema, Nakusihi, Ee BWANA, Mungu wa mbinguni, Mungu mkuu, mwenye kuogofya, mwenye kutimiza agano lake na rehema zake kwa hao wampendao na kuzishika amri zake;


Watu watayataja matendo yako ya kutisha, Nami nitausimulia ukuu wako.


Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote, Imbeni kwa zaburi.


Kwa mambo ya kutisha utatujibu, Katika haki, Ee Mungu wa wokovu wetu. Wewe uliye tumaini la miisho yote ya dunia, Na la bahari iliyo mbali sana,


Mungu ni mwenye kutisha Kutoka patakatifu pako. Ndiye Mungu wa Israeli; Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo. Na ahimidiwe Mungu.


Yeye huzikata roho za wakuu; Na kuwatisha wafalme wa dunia.


Kwa kuwa BWANA ni Mungu mkuu, Na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.


Na walisifu jina lake kuu litishalo; Ndiye mtakatifu.


Lakini na alaaniwe mtu adanganyaye, ambaye katika kundi lake ana dume, akaweka nadhiri, ila amtolea Bwana kitu kilicho na kilema; kwa maana mimi ni Mfalme mkuu, asema BWANA wa majeshi, na jina langu latisha katika mataifa.


Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.


Kama hutaki kutunza kufanya maneno yote ya torati hii yaliyoandikwa katika kitabu hiki, upate kulicha jina hili la fahari na utisho, BWANA, MUNGU WAKO;


Usiingiwe na hofu kwa sababu yao; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yuko pamoja nawe, Mungu mkuu, mwenye utisho.