BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonesha;
Zaburi 45:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Sikiliza binti, ufikirie! Tega sikio lako: Sahau sasa watu wako na jamaa zako. Biblia Habari Njema - BHND Sikiliza binti, ufikirie! Tega sikio lako: Sahau sasa watu wako na jamaa zako. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Sikiliza binti, ufikirie! Tega sikio lako: sahau sasa watu wako na jamaa zako. Neno: Bibilia Takatifu Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako. Neno: Maandiko Matakatifu Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako. BIBLIA KISWAHILI Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. |
BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonesha;
Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
Wakafika Ofiri, wakachukua toka huko dhahabu, talanta mia nne na ishirini, wakamletea mfalme Sulemani.
Naye akamwambia, Siendi mimi; ila nitairudia nchi yangu mwenyewe, na kwa jamaa zangu mwenyewe.
Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele.
Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake wa kiume na wa kike; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
Hata imekuwa, sisi tangu sasa hatumjui mtu awaye yote kwa jinsi ya mwili. Ingawa sisi tumemtambua Kristo kwa jinsi ya mwili, lakini sasa hatumtambui hivi tena.
Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.
avue na mavazi ya uteka wake akae nyumbani mwako, awakalie matanga babaye na mamaye mwezi mzima, kisha uingie kwake uwe mumewe, naye awe mkeo.
Aliyemtaja baba yake na mama yake, Mimi sikumwona; Wala nduguze hakuwakubali; Wala hakuwajua watoto wake mwenyewe; Maana wameliangalia neno lako, Wamelishika agano lako.