Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 37:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo, Utapaangalia mahali pake wala hatakuwapo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Bado kitambo kidogo, naye mwovu atatoweka; utamtafuta pale alipokuwa, wala hutamwona.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Bado kitambo kidogo, naye mwovu atatoweka; utamtafuta pale alipokuwa, wala hutamwona.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Bado kitambo kidogo, naye mwovu atatoweka; utamtafuta pale alipokuwa, wala hutamwona.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana, ingawa utawatafuta, hawataonekana.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana, ingawa utawatafuta, hawataonekana.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo, Utapaangalia mahali pake wala hatakuwepo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 37:10
25 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo Yehu akamwambia Bidkari, msaidizi wake, Mtwae ukamtupe katika kiwanja cha Nabothi, Myezreeli; maana kumbuka, hapo mimi na wewe tulipokuwa tumepanda farasi zetu, na kumfuata Anabu baba yake, BWANA alimwekea mzigo huu, akasema;


Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia.


Lakini mwanadamu hufa, hufariki dunia; Naam, mwanadamu hukata roho, naye yupo wapi?


Ya kuwa shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo, Na furaha ya wapotovu ni ya dakika moja tu?


Wao wametukuzwa; lakini kitambo kidogo hutoweka; Naam, hushushwa, na kuondolewa njiani kama wengine wote, Nao hukatwa kama vile masuke ya ngano.


Hatarudi tena nyumbani kwake, Wala mahali pake hapatamjua tena.


Nawe, je! Mbona hunisamehe makosa yangu, Na kuniondolea maovu yangu? Kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; Nawe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwapo.


Maana upepo hupita juu yake, na kutoweka! Lisionekane mahali lilipokuwa tena.


Naam, ataliona, hata wenye hekima hufa; Mpumbavu na mjinga hupotea pamoja, Na kuwaachia wengine mali zao.


Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung'oa katika nchi ya walio hai.


Nyumba ya mtu mwovu itabomolewa; Bali hema la mwenye haki litafanikiwa.


Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.