Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 35:22 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Wewe, BWANA, umeona, usinyamaze; Ee Bwana, usiwe mbali nami.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini wewe Mwenyezi-Mungu waona jambo hilo, usinyamaze, ee Mwenyezi-Mungu, usikae mbali nami.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini wewe Mwenyezi-Mungu waona jambo hilo, usinyamaze, ee Mwenyezi-Mungu, usikae mbali nami.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini wewe Mwenyezi-Mungu waona jambo hilo, usinyamaze, ee Mwenyezi-Mungu, usikae mbali nami.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ee Mwenyezi Mungu, umeona hili, usiwe kimya. Usiwe mbali nami, Ee Bwana.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ee bwana, umeona hili, usiwe kimya. Usiwe mbali nami, Ee bwana.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wewe, BWANA, umeona, usinyamaze; Ee Bwana, usiwe mbali nami.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 35:22
14 Marejeleo ya Msalaba  

Ee BWANA, kwa nini wasimama mbali? Kwani unajificha nyakati za shida?


Umeona, maana unaangalia matatizo na dhiki, Uyatwae mkononi mwako. Mtu duni hukuachia nafsi yake, Maana umekuwa msaidizi wa yatima.


Usiwe mbali nami maana taabu i karibu, Kwa maana hakuna msaidizi.


Mafahali wengi wamenizunguka, Walio hodari wa Bashani wamenisonga;


Nawe, BWANA, usiwe mbali, Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia.


Ee BWANA, nitakuita Ewe, mwamba wangu, Usiwe kwangu kama kiziwi. Nisije nikafanana nao washukao shimoni, Ikiwa umeninyamalia.


Wewe, BWANA, usiniache, Mungu wangu, usijitenge nami.


Ee BWANA, usikie maombi yangu, Utege sikio lako niliapo, Usiyapuuze machozi yangu. Kwa maana mimi ni mgeni wako, Msafiri kama baba zangu wote.


Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza; Ukadhani ya kuwa Mimi ni kama wewe. Lakini nitakukemea; Nitakuhukumu kwa hayo yote.


Ee Mungu, usiwe mbali nami; Ee Mungu wangu, fanya haraka kunisaidia.


Ee Mungu, usistarehe, Ee Mungu, usinyamae, wala usitulie.


BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;


Tazama, neno hili limeandikwa mbele zangu. Sitanyamaza, lakini nitalipa, naam, mimi nitawalipa ujira wao vifuani mwao;


Hakika nimeona mateso ya watu wangu waliomo Misri, nimesikia kuugua kwao, nami nimeshuka niwatoe. Basi sasa, nitakutuma mpaka Misri.