Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 34:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mwelekezeeni macho, mpate kufurahi, Na nyuso zenu hazitaaibishwa kamwe.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mgeukieni Mungu mpate kufurahi; nanyi hamtaaibishwa kamwe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mgeukieni Mungu mpate kufurahi; nanyi hamtaaibishwa kamwe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mgeukieni Mungu mpate kufurahi; nanyi hamtaaibishwa kamwe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mwelekezeeni macho, mpate kufurahi, Na nyuso zenu hazitaaibishwa kamwe.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 34:5
17 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Yoabu akaingia nyumbani kwa mfalme, akasema, Wewe leo umefedhehesha nyuso za watumishi wako wote, waliokuokoa leo roho yako, na roho za wanao, na za binti zako, na roho za wake zako, na roho za masuria wako;


Ikawa nuru na furaha na shangwe na heshima kwa Wayahudi.


Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti.


Siku ile niliyokuita uliniitikia, Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu.


Kwa kuwa Wewe unaiwasha taa yangu; BWANA Mungu wangu aniangazia giza langu.


Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja; Wataaibika watendao uhaini bila sababu.


Nilijilaza na kulala usingizi, kisha ninaamka tena, Kwa kuwa BWANA ananitegemeza.


Maana kwako Wewe iko chemchemi ya uzima, Katika nuru yako tutaona nuru.


Uniite siku ya mateso; Nitakuokoa, nawe utanitukuza.


Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, Nitamwonesha wokovu wa Mungu.


Uzijaze nyuso zao fedheha; Ili wapate kulitafuta jina lako, Ee BWANA.


Nuru humwangazia mwenye haki, Na furaha ni kwa wanyofu wa moyo.


Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.


Ndipo utakapoona na kutiwa nuru, Na moyo wako utatetemeka na kukunjuka; Kwa kuwa wingi wa bahari utageuzwa kukujia, Utajiri wa mataifa utakuwasilia.


tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi katika mkono wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.


Basi Daudi na watu wake, ambao walikuwa kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda popote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akauacha mpango wake.