Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 34:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nilimtafuta BWANA, naye akanijibu, Akaniokoa kutoka kwa hofu zangu zote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nilimwomba Mwenyezi-Mungu naye akanijibu, na kuniondoa katika hofu zangu zote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nilimwomba Mwenyezi-Mungu naye akanijibu, na kuniondoa katika hofu zangu zote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nilimwomba Mwenyezi-Mungu naye akanijibu, na kuniondoa katika hofu zangu zote.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nilimtafuta Mwenyezi Mungu naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nilimtafuta bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nilimtafuta BWANA, naye akanijibu, Akaniokoa na hofu zangu zote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 34:4
20 Marejeleo ya Msalaba  

naye akatoka ili amlaki Asa, akamwambia, Nisikieni, Ee Asa, na Yuda wote na Benyamini; BWANA yu pamoja nanyi, mkiwa pamoja naye; nanyi mkimtafuta ataonekana kwenu; lakini mkimwacha atawaacha ninyi.


Katika shida yangu nilimwita BWANA, Na kumlalamikia Mungu wangu. Akaisikia sauti yangu hekaluni mwake, Kilio changu kikaingia masikioni mwake.


Maana hapuuzi Wala kuchukizwa na mateso ya anayeteswa, Wala hamfichi uso wake, Bali humsikia akimlilia.


Nami nilisema kwa pupa yangu, Nimekatiliwa mbali na macho yako; Lakini ulisikia sauti ya kilio changu Wakati nilipokulilia.


Washangilie na kufurahi, Wapendezwao na haki yangu. Naam, waseme daima, Atukuzwe BWANA, Apendezwaye na amani ya mtumishi wake.


Nami ni maskini na mhitaji, Bwana atanitunza. Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, Ee Mungu wangu, usikawie.


Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.


Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;


Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana BWANA YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu.


Akasema, Nilimlilia BWANA kwa sababu ya shida yangu, Naye akaniitikia; Katika tumbo la kuzimu niliomba, Nawe ukasikia sauti yangu.


Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;


Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.


Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.


Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;


Ndipo Daudi aliposema moyoni mwake, Siku moja, basi, mimi nitaangamia kwa mkono wa Sauli; hakuna jema zaidi kwangu kuliko kukimbia mpaka nchi ya Wafilisti; naye Sauli atakata tamaa kunihusu, asinitafute tena kote mipakani mwa Israeli; hivyo nitaokoka katika mikono yake.