Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 34:19 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini BWANA kutoka kwayo yote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mateso ya mwadilifu ni mengi, lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mateso ya mwadilifu ni mengi, lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mateso ya mwadilifu ni mengi, lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Mwenyezi Mungu humwokoa nayo yote,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mwenye haki ana mateso mengi, lakini bwana humwokoa nayo yote,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini BWANA humponya na hayo yote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 34:19
24 Marejeleo ya Msalaba  

Basi hivyo BWANA akaubariki huo mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake; naye alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, na ngamia elfu sita, na jozi za ng'ombe elfu moja, na punda wake elfu moja.


Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.


Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuyaganga majeraha yao.


Walilia, naye BWANA akasikia, Akawaponya kutoka kwa taabu zao zote.


Nilimtafuta BWANA, naye akanijibu, Akaniokoa kutoka kwa hofu zangu zote.


Maskini huyu aliita, BWANA akasikia, Akamwokoa na taabu zake zote.


Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki, Na sadaka za kuteketezwa, na kafara. Ndipo watakapotoa ng'ombe Juu ya madhabahu yako.


Wewe, uliyetuonesha mateso mengi, mabaya, Utatuhuisha tena. Utatupandisha juu tena Kutoka katika vina virefu chini ya nchi.


Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.


Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yuko karibu;


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.


wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwahimiza wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi.


Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda mfupi tu, yatuandalia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana;


Akafa Elimeleki, mumewe Naomi; na yule mwanamke akasalia na wanawe wawili.