Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 32:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kimbilio langu utanilinda nisipate mateso, Utanizungusha nyimbo za kufurahia wokovu wangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wewe ndiwe kinga yangu; wewe wanilinda katika taabu. Umenijalia shangwe za kukombolewa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wewe ndiwe kinga yangu; wewe wanilinda katika taabu. Umenijalia shangwe za kukombolewa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wewe ndiwe kinga yangu; wewe wanilinda katika taabu. Umenijalia shangwe za kukombolewa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha, utaniepusha na taabu na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha, utaniepusha na taabu na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kimbilio langu utanilinda nisipate mateso, Utanizungusha nyimbo za kufurahia wokovu wangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 32:7
18 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Daudi akamwambia BWANA maneno ya wimbo huu, siku ile BWANA alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na mkononi mwa Sauli;


Ndiwe sitara yangu na ngao yangu, Neno lako nimelingojea.


Ee BWANA, uniponye kutoka kwa adui zangu; Nimekukimbilia Wewe, unifiche.


Kamba za kuzimu zilinizunguka, Mitego ya mauti ikanikabili.


Maana atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya, Atanisitiri katika sitara ya hema yake, Na kuniinua juu ya mwamba.


Utawasitiri kutoka kwa fitina za watu Katika maficho ya kuwapo kwako; Utawaficha katika hema Na ushindani wa ndimi.


Naye mtu mwovu ana mapigo mengi, Bali amtumainiaye BWANA fadhili zitamzunguka.


Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumainia BWANA.


Kwa maana Wewe utambariki mwenye haki; BWANA, utamzungushia radhi kama ngao.


BWANA atakuwa ngome kwake aliyeonewa, Naam, ngome kwa nyakati za shida.


Aketiye mahali pa siri pake Aliye Juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.


Mwimbieni BWANA wimbo mpya, Kwa maana ametenda mambo ya ajabu. Mkono wa kulia, Na mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu.


Mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, na Seraya, mwana wa Azrieli, na Shelemia, mwana wa Abdeeli, wamkamate Baruku, mwandishi, na Yeremia, nabii; lakini BWANA aliwaficha.


Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.


wakilia kwa sauti kuu wakisema, Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-kondoo.


Ndipo Debora, na Baraka mwana wa Abinoamu, wakaimba siku ile, wakisema;