Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 31:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ndiwe mwamba wangu na ngome yangu; Kwa ajili ya jina lako uniongoze na unichunge.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Naam, wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hisani yako uniongoze na kunielekeza.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Naam, wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hisani yako uniongoze na kunielekeza.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Naam, wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hisani yako uniongoze na kunielekeza.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu, uniongoze na kunilinda kwa ajili ya jina lako.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu, uniongoze na kunilinda kwa ajili ya jina lako.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ndiwe mwamba wangu na ngome yangu; Kwa ajili ya jina lako uniongoze na unichunge.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 31:3
21 Marejeleo ya Msalaba  

Zaidi ya hayo ukawaongoza kwa nguzo ya wingu mchana; na kwa nguzo ya moto usiku; ili kuwapa mwanga katika njia iliyowapasa kuiendea.


hata hivyo wewe kwa wingi wa rehema zako hukuwaacha jangwani; nguzo ya wingu haikuondoka kwao wakati wa mchana, ili kuwaongoza njiani; wala nguzo ya moto haikuondoka wakati wa usiku, ili kuwapa mwanga na kuwaonesha njia watakayoiendea.


Maana siku zangu zinatoweka kama moshi, Na mifupa yangu inateketea kama kinga.


Kwa maana amenitegea sikio lake, Kwa hiyo nitamwita siku zangu zote.


Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele.


BWANA ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu, Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.


Ee BWANA, kwa ajili ya jina lako, Unisamehe uovu wangu, maana ni mwingi.


Uniongoze katika kweli yako, Na kunifundisha. Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, Nakungoja Wewe mchana kutwa.


Wenye upole atawaongoza katika haki, Wenye upole atawafundisha njia yake.


Nitumie nuru yako na kweli yako ziniongoze, Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata katika maskani yako.


Uwe kwangu mwamba wa makazi yangu, Ngome imara ya wokovu wangu. Maana wewe, Ndiwe mwamba wangu na ngome yangu.


Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie, Kwa ajili ya utukufu wa jina lako. Utuokoe, utusamehe dhambi zetu, Kwa ajili ya jina lako.


Hawataona njaa, wala hawataona kiu; joto halitawapiga, wala jua; kwa maana yeye aliyewarehemu atawatangulia, naam, karibu na chemchemi za maji atawaongoza.


Ijapokuwa maovu yetu yanatushuhudia, lakini utende wewe kwa ajili ya jina lako, Ee BWANA, maana kurudi nyuma kwetu ni kwingi; tumekutenda dhambi.


Kuwaangaza wakaao katika giza na uvuli wa mauti, Na kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.


Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.


Nasi katika huyo tupate kuwa sifa ya utukufu wake, sisi tuliotangulia kumwekea Kristo tumaini letu.


Maana Wakanaani na wenyeji wote wa nchi hii watasikia habari hii, nao watatuzingira, na kulifuta jina letu katika nchi. Nawe utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?