Umeona, maana unaangalia matatizo na dhiki, Uyatwae mkononi mwako. Mtu duni hukuachia nafsi yake, Maana umekuwa msaidizi wa yatima.
Zaburi 26:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Mikononi mwao mna madhara, Na mkono wao wa kulia umejaa rushwa. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema watu ambao matendo yao ni maovu daima, watu ambao wamejaa rushwa. Biblia Habari Njema - BHND watu ambao matendo yao ni maovu daima, watu ambao wamejaa rushwa. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza watu ambao matendo yao ni maovu daima, watu ambao wamejaa rushwa. Neno: Bibilia Takatifu ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa. Neno: Maandiko Matakatifu ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa. BIBLIA KISWAHILI Mikononi mwao mna madhara, Na mkono wao wa kuume umejaa rushwa. |
Umeona, maana unaangalia matatizo na dhiki, Uyatwae mkononi mwako. Mtu duni hukuachia nafsi yake, Maana umekuwa msaidizi wa yatima.
Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.
Nawe usipokee rushwa; kwani hiyo rushwa huwapofusha macho hao waonao, na kuyapotoa maneno ya wenye haki.
Maana hawalali isipokuwa wametenda madhara; Huondolewa usingizi, ikiwa hawakumwangusha mtu.
Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung'utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za umwagaji wa damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
Maana mimi najua jinsi maasi yenu yalivyo mengi, na jinsi dhambi zenu zilivyo kubwa; ninyi mnaowaonea wenye haki, mnaopokea rushwa, na kuwageuza wahitaji langoni wasipate haki yao.
Mikono yao ni hodari kwa kutenda maovu; afisa na hakimu wanataka rushwa, mtu mkubwa hunena madhara yaliyomo rohoni mwake; hivyo ndivyo wayafumavyo hayo pamoja.
Kulipopambazuka, Wayahudi wakafanya mapatano, wakajifunga kwa kiapo kwamba hawatakula wala hawatakunywa hadi wamwue Paulo.
Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza kesi wa wenye haki.
Ila wanawe hawakuenda katika njia zake, bali waliziacha, ili wapate faida; wakapokea rushwa, na kupotosha hukumu.