Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 22:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Wote wanionao hunicheka sana, Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wote wanionao hunidhihaki; hunifyonya na kutikisa vichwa vyao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wote wanionao hunidhihaki; hunifyonya na kutikisa vichwa vyao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wote wanionao hunidhihaki; hunifyonya na kutikisa vichwa vyao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wote wanaoniona wananidhihaki; wananivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wote wanionao hunicheka sana, Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 22:7
22 Marejeleo ya Msalaba  

Mimi ni mtu wa kuchekwa na jirani yake, Ni mtu niliyemwita Mungu, naye akanijibu; Huyo mwenye haki, aliye mtimilifu, amekuwa ni kicheko.


Wamenifumbulia vinywa vyao; Wamenipiga shavuni kwa kunitukana; Hukutana pamoja juu yangu.


Mimi nami ningeweza kunena kama ninyi; Kama roho zenu zingekuwa mahali pa roho yangu, Ningeweza kutunga maneno juu yenu, Na kuwatikisia ninyi kichwa changu.


Nami nimekuwa wa kudharauliwa na watu, Wanionapo hutikisa vichwa vyao.


Midomo ya uongo iwe na ububu, Imneneayo mwenye haki maneno ya kiburi, Kwa majivuno na dharau.


Umetufanya kuwa mithali kwa mataifa, Sababu ya kutikisa kichwa kwa watu wa nchi.


BWANA, mkombozi wa Israeli, Mtakatifu wake, amwambia hivi yeye anayedharauliwa na wanadamu; yeye anayechukiwa na taifa hili; yeye aliye mtumishi wao watawalao; Wafalme wataona, watasimama; wakuu nao watasujudu; kwa sababu ya BWANA aliye mwaminifu, Mtakatifu wa Israeli aliyekuchagua.


Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.


Mnafanya dhihaka yenu juu ya nani? Mmepanua vinywa vyenu, na kutoa ndimi zenu? Je, ninyi si wana wa uasi, uzao wa uongo;


Wakasokota taji la miiba, wakaliweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kulia; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!


akawaambia, Ondokeni; kwa maana msichana hakufa, amelala tu. Wakamcheka sana.


Hata wakiisha kumdhihaki, wakamvua lile vazi la rangi ya zambarau, wakamvika mavazi yake mwenyewe; wakampeleka nje ili wamsulubishe.


Nao waliokuwa wakipita njiani wakamtukana, wakitikisatikisa vichwa, wakisema, Ahaa! Wewe mwenye kulivunja hekalu na kulijenga katika siku tatu,


Basi Mafarisayo, ambao wenyewe ni wapenda fedha, waliyasikia hayo yote, wakamdhihaki.


Basi Herode akamdhalilisha, pamoja na askari wake, akamdhihaki, na kumvika mavazi mazuri; kisha akamrudisha kwa Pilato.