Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 22:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mafahali wengi wamenizunguka, Walio hodari wa Bashani wamenisonga;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Maadui wengi wanizunguka kama fahali; wamenisonga kama fahali wakali wa Bashani!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Maadui wengi wanizunguka kama fahali; wamenisonga kama fahali wakali wa Bashani!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Maadui wengi wanizunguka kama fahali; wamenisonga kama fahali wakali wa Bashani!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mafahali wengi wamenizunguka, Walio hodari wa Bashani wamenisonga;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 22:12
14 Marejeleo ya Msalaba  

Wewe, BWANA, umeona, usinyamaze; Ee Bwana, usiwe mbali nami.


Ufanye haraka kunisaidia, Ee Bwana, wokovu wangu.


Waaibike na wafedheheke, Wote wanaotaka kuniua. Warudishwe nyuma, watahayarishwe, Wapendezwao na shari yangu.


Mkemee mnyama wa mafunjoni; Kundi la mafahali, na ndama za watu; Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha, Uwatawanye watu wapendao vita.


Uikaribie nafsi yangu, uikomboe, Kwa sababu ya adui zangu unifidie.


BWANA, Mungu wangu, ikiwa nimetenda haya, Ikiwa mna uovu mikononi mwangu,


Waaibike, wafedheheke, Wanaoitafuta nafsi yangu. Warudishwe nyuma, watahayarishwe, Wapendezwao na shari yangu.


Na nyati watateremka pamoja nao, na ndama pamoja na mafahali, na nchi yao italewa kwa damu, na mavumbi yake yatanoneshwa kwa shahamu.


Kwa sababu mnafurahi, kwa sababu mnashangilia, enyi mnaouteka urithi wangu, kwa sababu mmenona kama mtamba akanyagaye nafaka, nanyi mnalia kama farasi wenye nguvu;


Mtakula nyama yao walio hodari, na kunywa damu ya wakuu wa dunia, ya kondoo dume na ya wana-kondoo, na ya mbuzi, na ya ng'ombe, wote na wanono wa Bashani.


Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua;


Maana ni kweli, Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta,