Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 21:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Utukufu wake ni mkuu kwa wokovu wako, Heshima na adhama waweka juu yake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kwa msaada wako ametukuka sana; wewe umemjalia fahari na heshima.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kwa msaada wako ametukuka sana; wewe umemjalia fahari na heshima.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kwa msaada wako ametukuka sana; wewe umemjalia fahari na heshima.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kutokana na ushindi uliompa, utukufu wake ni mkubwa, umeweka juu yake fahari na utukufu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kutokana na ushindi uliompa, utukufu wake ni mkubwa, umeweka juu yake fahari na utukufu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Utukufu wake ni mkuu kwa wokovu wako, Heshima na adhama waweka juu yake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 21:5
24 Marejeleo ya Msalaba  

Tena jambo hili lilikuwa dogo machoni pako, Ee Bwana MUNGU; hata umeleta habari ya nyumba yangu mimi, mtumishi wako, kwa miaka mingi inayokuja baadaye; na hayo kwa namna ya kibinadamu, Ee Bwana MUNGU.


Nawe ukienda katika njia zangu, na kuyashika mausia yangu, na amri zangu, kama baba yako Daudi alivyokwenda, basi nitazifanya siku zako kuwa nyingi.


nawe sasa umekuwa radhi kuibarikia nyumba ya mtumishi wako, ipate kudumu milele mbele zako; kwa maana wewe, BWANA, umebarikia, nayo imebarikiwa milele.


Neno la BWANA kwa Bwana wangu, Uketi upande wangu wa kulia, Hadi niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako.


Ni kama umande wa Hermoni ushukao milimani pa Sayuni. Maana huko ndiko BWANA alikoamuru baraka, Naam, uzima hata milele.


Lakini Wewe, BWANA, U ngao yangu pande zote, Utukufu wangu na mwinua kichwa changu.


Atakaa mbele za Mungu milele, Ziagize fadhili na kweli zimhifadhi.


Kwa Mungu wokovu wangu, Na utukufu wangu; Mwamba wa nguvu zangu, Na kimbilio langu ni kwa Mungu.


Umemfanya mdogo kuliko Mungu; Umemvika taji la utukufu na heshima;


Heshima na adhama ziko mbele zake, Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.


Ni nani huyu atokaye Edomu, Atokaye Bosra akiwa na mavazi yenye madoa mekundu? Huyu aliye na nguo za fahari, Anayekwenda katika ukuu wa uweza wake? Ndimi nisemaye kwa haki, Niliye hodari wa kuokoa.


Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.


Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe;


Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.


Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.


Basi, katika hayo tunayosema, neno lililo kuu ndilo hili: Tunaye kuhani mkuu wa namna hii, aliyeketi mkono wa kulia wa kiti cha enzi cha Ukuu mbinguni,


Naye yuko katika mkono wa kulia wa Mungu, amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.