Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 2:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Utawaponda kwa fimbo ya chuma, Na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Utawaponda kwa fimbo ya chuma; utawavunja kama chungu cha mfinyanzi!’”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Utawaponda kwa fimbo ya chuma; utawavunja kama chungu cha mfinyanzi!’”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Utawaponda kwa fimbo ya chuma; utawavunja kama chungu cha mfinyanzi!’”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Utawapondaponda kwa fimbo ya chuma, na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Utawaponda kwa fimbo ya chuma, Na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 2:9
14 Marejeleo ya Msalaba  

Bali nitawaponda watesi wake mbele yake, Nitawapiga wanaomchukia.


Naye atapavunja kama chombo cha mfinyanzi kivunjwavyo, kinavyovunjwavunjwa kikatili, hata hakipatikani katika vipande vyake kigae kitoshacho kutwaa moto jikoni, au kuteka maji kisimani.


Kwa maana kila taifa na ufalme wa watu Wasiotaka kukutumikia wataangamia; Naam, mataifa hayo wataharibiwa kabisa.


Nitawagonganisha, mtu na mwenzake, naam, baba za watu na watoto wao pamoja, asema BWANA; sitahurumia, wala sitaachilia, wala sitarehemu, hata nisiwaangamize.


na kuwaambia, BWANA wa majeshi asema hivi, Hivyo ndivyo nitakavyowavunja watu hawa, na mji huu, kama mtu avunjavyo chombo cha mfinyanzi, kisichoweza kutengenezwa tena na kuwa kizima; nao watazika watu katika Tofethi hata pasibaki mahali pa kuzikia.


Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.


Na kama vile ulivyoona ya kuwa jiwe lilichongwa mlimani bila kazi ya mikono, na ya kuwa lilivunjavunja kile chuma, na ile shaba na ule udongo, na ile fedha, na ile dhahabu; basi Mungu aliye mkuu amemjulisha mfalme mambo yatakayokuwa baadaye; na ndoto hii ni ya hakika, na tafsiri yake ni thabiti.


Na hayo mabaki ya Yakobo yatakuwa kati ya mataifa, kati ya kabila nyingi, mfano wa simba kati ya wanyama wa msituni, kama mwanasimba kati ya makundi ya kondoo, ambaye, akiwa anapita katikati, hukanyagakanyaga na kuraruararua, wala hakuna wa kuokoa.


Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vipande vipande; naye yeyote ambaye litamwangukia, litamsaga tikitiki.


Naye akazaa mtoto wa kiume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hadi kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi.


Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili kwa upanga huo awapige mataifa. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.