Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 2:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Yeye aketiye mbinguni anacheka, Bwana anawafanyia dhihaka.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwenyezi-Mungu atawalaye juu mbinguni, anawacheka na kuwadhihaki.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwenyezi-Mungu atawalaye juu mbinguni, anawacheka na kuwadhihaki.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenyezi-Mungu atawalaye juu mbinguni, anawacheka na kuwadhihaki.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Yeye anayetawala mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yeye aketiye mbinguni anacheka, Bwana anawafanyia dhihaka.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 2:4
13 Marejeleo ya Msalaba  

Tamko alilolitamka BWANA katika habari zake ndilo hili, Bikira, binti Sayuni, amekudharau, na kukudhihaki sana; binti Yerusalemu ametikisa kichwa chake juu yako.


BWANA yu katika hekalu lake takatifu. BWANA ambaye kiti chake kiko mbinguni, Macho yake yanaangalia; Kope zake zinawapima wanadamu.


Lakini Mungu wetu yuko mbinguni, Alitakalo lote amelitenda.


Nimekuinulia macho yangu, Wewe uketiye mbinguni.


BWANA atamcheka, Maana ameona kwamba siku yake inakuja.


Hapo waliingiwa na hofu pasipokuwapo hofu, Maana Mungu ameitawanya mifupa yake aliyekuhusuru. Umewatia aibu, Kwa sababu MUNGU amewadharau.


Na Wewe, BWANA, utawacheka, Utawadhihaki mataifa yote.


Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu.


Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele; Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.


Mimi nami nitacheka siku ya msiba wenu, Nitadhihaki hofu yenu ifikapo;


Yeye ndiye anayeketi juu ya duara ya dunia, na hao wanaokaa ndani yake huwa kama panzi; yeye ndiye azitandazaye mbingu kama pazia na kuzikunjua kama hema ya kukaliwa;


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?