Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 19:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ni nani awezaye kuyatambua makosa yake? Unitakase na mambo ya siri.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini nani aonaye makosa yake mwenyewe? Ee Mungu, niepushe na makosa nisiyoyajua.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini nani aonaye makosa yake mwenyewe? Ee Mungu, niepushe na makosa nisiyoyajua.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini nani aonaye makosa yake mwenyewe? Ee Mungu, niepushe na makosa nisiyoyajua.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ni nani awezaye kuyatambua makosa yake? Unitakase na mambo ya siri.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 19:12
19 Marejeleo ya Msalaba  

Nifunzeni, nami nitanyamaa kimya; Mkanijulishe ni jambo gani nililokosa.


Wewe wajua kuketi kwangu na kusimama kwangu; Umelifahamu wazo langu tokea mbali.


Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi, Hayadirikiki, siwezi kuyafikia.


Kwa maana mabaya yasiyohesabika Yamenizunguka mimi. Maovu yangu yamenipata, Wala siwezi kuona. Yamezidi kuliko nywele za kichwa changu, Nami nimevunjika moyo.


Unioshe kabisa uovu wangu, Unitakase dhambi zangu.


Tutakapozidiwa na matendo maovu Wewe utatuondolea uovu wetu.


Umeyaweka maovu yetu mbele zako, Dhambi zetu za siri katika mwanga wa uso wako.


BWANA akamwambia Musa, Njoo huku juu kwangu mlimani, uwe huku; nami nitakupa vibao vya mawe na ile sheria na hiyo amri niliyoiandika ili uwafundishe.


Kila anayelidharau neno hujiletea uharibifu; Bali yeye anayeiogopa amri atapewa thawabu.


Kwa maana sisi sote tumekuwa kama mtu aliye mchafu, na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo iliyotiwa unajisi; sisi sote twanyauka kama jani, na maovu yetu yatuondoa, kama upepo uondoavyo.


Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?


Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana.


Laiti wangekuwa na moyo kama huu ndani yao sikuzote, wa kunicha, na kushika amri zangu zote sikuzote, wapate kufanikiwa wao na watoto wao milele!


Tunzeni basi, mtende kama mlivyoamriwa na BWANA, Mungu wenu; msikengeuke kwa mkono wa kulia wala wa kushoto.


Lakini katika hema hiyo ya pili kuhani mkuu huingia peke yake, mara moja kila mwaka; wala si pasipo damu, atoayo kwa ajili ya nafsi yake na kwa dhambi walizozitenda hao watu bila kujua.


bali tukienenda katika nuru, kama yeye alivyo katika nuru, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.