Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 18:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kamba za mauti zilinizunguka, Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kamba za kifo zilinizingira, mawimbi ya maangamizi yalinivamia;

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kamba za kifo zilinizingira, mawimbi ya maangamizi yalinivamia;

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kamba za kifo zilinizingira, mawimbi ya maangamizi yalinivamia;

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kamba za mauti zilinizunguka, Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 18:4
18 Marejeleo ya Msalaba  

Naye alipokwisha kufanya shauri na watu, akawaweka wale watakaomwimbia BWANA, na kumsifu katika uzuri wa utakatifu, wakitoka mbele ya jeshi, na kusema, Mshukuruni BWANA; kwa maana fadhili zake ni za milele.


Nao walipoanza kuimba na kusifu, BWANA akaweka waviziao juu ya Waamoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, waliokuja kushambulia Yuda; nao wakapigwa.


Kamba za mauti zilinizunguka, Shida za kuzimu zilinipata. Nilipata dhiki na mateso;


Papo hapo maji yangalitugharikisha, Mto ungalipita juu ya roho zetu;


Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenidunga mikono na miguu.


Nao watafadhaika; watashikwa na uchungu na maumivu; watakuwa na uchungu kama mwanamke aliye karibu kuzaa; watakodoleana macho; nyuso zao zitakuwa ni nyuso za moto.


Basi alipokuwa katika kusema, tazama, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili akaja, na pamoja naye kundi kubwa wenye panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani na wazee wa watu.


Saa ile Yesu akawaambia makutano, Je, mmetoka kama kumkamata mnyang'anyi, wenye panga na marungu, ili kunishika? Kila siku niliketi hekaluni nikifundisha, msinikamate.


Mji wote ukataharuki, watu wakakutanika mbio mbio, wakamkamata Paulo, wakamkokota, wakamtoa hekaluni; mara milango ikafungwa.


Naam, sisi wenyewe tulikuwa na hukumu ya mauti katika nafsi zetu ili tusijitumainie nafsi zetu, bali tumtumaini Mungu, awafufuaye wafu,