Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 18:27 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Maana Wewe wawaokoa watu wanaoonewa, Na macho ya kiburi utayadhili.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wewe wawaokoa walio wanyenyekevu, lakini wenye majivuno huwaporomosha.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wewe wawaokoa walio wanyenyekevu, lakini wenye majivuno huwaporomosha.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wewe wawaokoa walio wanyenyekevu, lakini wenye majivuno huwaporomosha.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maana Wewe wawaokoa watu wanaoonewa, Na macho ya kiburi utayadhili.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 18:27
20 Marejeleo ya Msalaba  

Na watu wanaoonewa wewe utawaokoa; Ila macho yako huwapinga wenye kiburi, uwadhili.


Mdhalimu kwa kiburi cha uso wake Asema, Mungu Hatapatiliza. Mawazo yake yote ni, Hakuna Mungu;


Amsingiziaye jirani yake kwa siri, Huyo nitamwangamiza. Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno, Huyo sitamvumilia.


Wamejawa na ukaidi, Kwa vinywa vyao wanajigamba.


Inuka, Ee BWANA, umkabili, umwangushe, Kwa upanga wako uniokoe nafsi yangu na mtu mbaya.


Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini BWANA kutoka kwayo yote.


Maskini huyu aliita, BWANA akasikia, Akamwokoa na taabu zake zote.


Nami ni maskini na mhitaji, Bwana atanitunza. Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, Ee Mungu wangu, usikawie.


Kwa maana mhitaji hatasahauliwa daima; Matumaini ya wanyonge hayatapotea milele.


Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe; Ambao hawakuoshwa uchafu wao.


Basi, itakuwa, Bwana atakapokuwa ameitimiza kazi yake yote juu ya mlima Sayuni na juu ya Yerusalemu, nitamwadhibu matunda ya kiburi cha moyo wake mfalme wa Ashuru, na majivuno ya macho yake.


Kuonekana kwa nyuso zao kwashuhudia juu yao, wafunua dhambi yao kama Sodoma, hawaifichi. Ole wa nafsi zao, kwa maana wamejilipa nafsi zao uovu.


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.


Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako.


Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.


Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao?