Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 16:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

BWANA ndiye fungu la posho langu, Na la kikombe changu; Wewe unayaamua maisha yangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wewe ee Mwenyezi-Mungu ndiwe riziki yangu kuu, majaliwa yangu yamo mikononi mwako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wewe ee Mwenyezi-Mungu ndiwe riziki yangu kuu, majaliwa yangu yamo mikononi mwako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wewe ee Mwenyezi-Mungu ndiwe riziki yangu kuu, majaliwa yangu yamo mikononi mwako.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mwenyezi Mungu umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

BWANA ndiye fungu la posho langu, Na la kikombe changu; Wewe unayaamua maisha yangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 16:5
28 Marejeleo ya Msalaba  

Awanyeshee wasio haki mitego, Moto na kiberiti na upepo wa joto Na viwe fungu la kikombe chao.


Nitakipokea kikombe cha wokovu; Na kulitangaza jina la BWANA;


BWANA ndiye aliye fungu langu, Ninaahidi kuyatii maneno yake.


Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya nchi ya wenye haki; Ili wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu.


BWANA amemwapia Daudi neno la kweli, Hatarudi nyuma akalivunja, Mmoja wa wazawa wako mwenyewe Nitawaweka katika kiti chako cha enzi.


BWANA, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu, Fungu langu katika nchi ya walio hai.


Nami nimemweka mfalme wangu Juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.


Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.


Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele.


Wazao wako nitawaimarisha milele, Nitakijenga kiti chako cha enzi hata milele.


Kwa maana umenifanyia hukumu na haki Umeketi kitini pa enzi ukihukumu kwa haki.


Tazama mtumishi wangu nimtegemezaye; mteule wangu, ambaye nafsi yangu imependezwa naye; nimetia roho yangu juu yake; naye atawatolea mataifa hukumu.


Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu, Naye atagawana nyara pamoja nao walio hodari; Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, Akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini alichukua dhambi za watu wengi, Na kuwaombea wakosaji.


Yeye, Fungu la Yakobo, siye kama hawa; Maana ndiye aliyeviumba vitu vyote; Na Israeli ni kabila la urithi wake; BWANA wa majeshi ndilo jina lake.


BWANA ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye.


Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.


Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kulia, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.


Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke adui zake wote chini ya miguu yake.


Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;


Wala wasiwe na urithi kati ya ndugu zao; BWANA ndiye urithi wao, kama alivyowaambia.


Maana, sehemu ya BWANA ni watu wake, Yakobo ni kura ya urithi wake.


Kwa kuwa yeye BWANA ameufanya huu mto wa Yordani uwe mpaka katikati yetu nanyi, enyi wana wa Reubeni, na wana wa Gadi, hamna fungu katika BWANA; basi hivyo wana wenu wangeweza kuwafanya wana wetu waache kumwabudu BWANA.


bali iwe ushahidi kati yetu nanyi, tena kati ya vizazi vyetu baada yetu, kwamba sisi tunamhudumia BWANA kwa njia ya sadaka zetu za kuteketezwa, na kwa dhabihu zetu, na kwa sadaka zetu za amani; ili kwamba wana wenu wasiwaambie wana wetu katika siku zijazo, Ninyi hamna fungu katika BWANA.