Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 150:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Msifuni kwa kupiga matoazi. Msifuni kwa matoazi ya sauti kubwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Msifuni kwa kupiga matoazi. Msifuni kwa matoazi ya sauti kubwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Msifuni kwa kupiga matoazi. msifuni kwa matoazi ya sauti kubwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 150:5
9 Marejeleo ya Msalaba  

Daudi na nyumba yote ya Israeli wakacheza mbele za BWANA kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa kayamba, na kwa matoazi.


Wakacheza Daudi na Israeli wote, mbele za Mungu, kwa nguvu zao zote; na kwa nyimbo na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa matoazi, na kwa tarumbeta.


Kisha Daudi akamwambia mkuu wa Walawi, kwamba awaagize ndugu zao waimbaji, pamoja na vyombo vyao vya kupigia ngoma, vinanda, na vinubi, na matoazi, wavipige na kupaza sauti kwa furaha.


Hivyo hao waimbaji, Hemani, Asafu, na Ethani, wakaagizwa kupiga matoazi yao ya shaba kwa sauti kuu;


Ndivyo Israeli wote walivyolipandisha sanduku la Agano la BWANA kwa shangwe na kwa sauti ya tarumbeta, na kwa baragumu, na kwa matoazi, wakipiga sauti kuu kwa vinanda na vinubi.


Asafu mkuu wao, na wa pili wake Zekaria, na Yeieli, na Shemiramothi, na Yehieli, na Metithia, na Eliabu, na Benaya, na Obed-edomu, na Yeieli, wenye vinanda na vinubi; naye Asafu mwenye kupiga matoazi;


Tena Daudi na makamanda wa jeshi wakatenga kwa utumishi baadhi ya wana wa Asafu, na wa Hemani, na wa Yeduthuni, watakaotabiri kwa vinubi na vinanda, na matoazi; hii ndiyo hesabu ya wafanya kazi kulingana na utumishi wao;


Hao wote waliamriwa na baba yao, waimbe nyumbani mwa BWANA, wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi, kwa utumishi wa nyumba ya Mungu; Asafu, Yeduthuni, na Hemani wakiwa wanaamriwa na mfalme.


hata ikawa, wenye panda na waimbaji walipokuwa kama mmoja, wakisikizisha sauti moja ya kumsifu na kumshukuru BWANA nao wakipaza sauti pamoja na panda na matoazi na vinanda, wakimsifu BWANA, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele; ndipo nyumba ikajawa na wingu, naam, nyumba ya BWANA,