Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 149:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa sauti tamu ya matari na kinubi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lisifuni jina lake kwa ngoma, mwimbieni kwa ngoma na zeze.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lisifuni jina lake kwa ngoma, mwimbieni kwa ngoma na zeze.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lisifuni jina lake kwa ngoma, mwimbieni kwa ngoma na zeze.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa sauti tamu ya matari na kinubi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 149:3
19 Marejeleo ya Msalaba  

Daudi akacheza mbele za BWANA kwa nguvu zake zote; na Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani.


Ikawa, sanduku la BWANA lilipoingia mji wa Daudi, Mikali binti Sauli, akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za BWANA; akamdharau moyoni mwake.


na pamoja nao Hemani na Yeduthuni wenye baragumu na matoazi, kwa hao watakaovumisha sauti, na vinanda kwa ajili ya hizo nyimbo za Mungu; na hao wana wa Yeduthuni wawepo mlangoni.


Hao wote waliamriwa na baba yao, waimbe nyumbani mwa BWANA, wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi, kwa utumishi wa nyumba ya Mungu; Asafu, Yeduthuni, na Hemani wakiwa wanaamriwa na mfalme.


Wakafika Yerusalemu wenye vinanda, vinubi na parapanda kwenda nyumbani kwa BWANA.


Akawasimamisha Walawi nyumbani mwa BWANA wenye matoazi, wenye vinanda, na wenye vinubi, kama alivyoamuru Daudi, na Gadi mwonaji wa mfalme, na Nathani nabii; kwani BWANA aliamuru hivi kwa manabii wake.


Hata wajenzi walipouweka msingi wa hekalu la BWANA, wakawaweka makuhani, wamevaa mavazi yao, wenye baragumu, na Walawi, wana wa Asafu, wenye matoazi, ili wamhimidi BWANA, kama alivyoagiza Daudi, mfalme wa Israeli.


Umegeuza msiba wangu kuwa ngoma; Umeniondolea huzuni yangu, kunijalia furaha tele.


Mshukuruni BWANA kwa kinubi, Kwa kinanda cha nyuzi kumi mwimbieni sifa.


Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.


Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Kukiwa na mbalamwezi, wakati wa sikukuu yetu.


Waimbao na wachezao ngoma na waseme, Visima vyangu vyote vimo mwako.


Na Miriamu, nabii mwanamke, dada yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza.


Ndipo bikira atafurahi katika kucheza, na vijana na wazee pamoja; maana nitageuza masikitiko yao kuwa furaha, nami nitawafariji, na kuwafurahisha waache huzuni zao.


Mara ya pili nitakujenga, nawe utajengwa, Ee bikira wa Israeli mara ya pili utapambwa kwa matari yako, nawe utatokea katika michezo yao wanaofurahi.


Kisha Yeftha akafika Mispa nyumbani kwake, na tazama, binti yake akamtokea kumlaki, na matari na akichezacheza; naye alikuwa ni mwanawe wa pekee; hakuwa na mwingine, wa kiume wala binti.