Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 142:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Utazame mkono wangu wa kulia ukaone, Kwa maana sina mtu anijuaye. Makimbilio yamenipotea, Hakuna wa kunitunza roho.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nikiangalia upande wa kulia na kungojea, naona hakuna mtu wa kunisaidia; sina tena mahali pa kukimbilia, hakuna mtu anayenijali.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nikiangalia upande wa kulia na kungojea, naona hakuna mtu wa kunisaidia; sina tena mahali pa kukimbilia, hakuna mtu anayenijali.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nikiangalia upande wa kulia na kungojea, naona hakuna mtu wa kunisaidia; sina tena mahali pa kukimbilia, hakuna mtu anayenijali.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Utazame mkono wangu wa kuume ukaone, Kwa maana sina mtu anijuaye. Makimbilio yamenipotea, Hakuna wa kunitunza roho.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 142:4
19 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini macho ya waovu yataingia kiwi, Nao hawatakuwa na njia ya kukimbilia, Na matumaini yao yatakuwa ni kutoa roho.


Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.


Nimemwambia BWANA, Ndiwe Mungu wangu; Ee BWANA, uisikie sauti ya dua zangu.


Unilinde kutoka kwa mtego walionitegea, Na kutoka kwa matanzi ya watendao maovu.


Na roho yangu imezimia ndani yangu, Moyo wangu ndani yangu umeshtuka.


Kwa sababu ya watesi wangu nimelaumiwa, Naam, hasa kwa jirani zangu; Na kitu cha kutisha kwa rafiki zangu; Wanaoniona njiani wananikimbia.


Laumu imenivunja moyo, Nami ninaugua sana. Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna; Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu.


Mpenzi na rafiki umewatenga nami, Nao wanijuao wamo gizani.


Wanijuao umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka.


Kilio na kisikiwe kitokacho katika nyumba zao, hapo utakapoleta kikosi juu yao kwa ghafla; kwa maana wamenichimbia shimo waninase, nao wameifichia miguu yangu mitego.


Nao wachungaji watakuwa hawana njia ya kukimbia, wala walio hodari katika kundi hawataokoka.


Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya majeraha yako, asema BWANA, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, mji ambao hakuna mtu autakaye.


Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongo Hujitenga na rehema zao wenyewe.


Lakini haya yote yamekuwa, ili maandiko ya manabii yatimizwe. Ndipo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.


Katika utetezi wangu wa kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu, bali wote waliniacha; naomba wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.


Ndipo Daudi aliposema moyoni mwake, Siku moja, basi, mimi nitaangamia kwa mkono wa Sauli; hakuna jema zaidi kwangu kuliko kukimbia mpaka nchi ya Wafilisti; naye Sauli atakata tamaa kunihusu, asinitafute tena kote mipakani mwa Israeli; hivyo nitaokoka katika mikono yake.