Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 141:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Afadhali mtu mwema anipige kunionya; lakini sikubali kamwe kusifiwa na wabaya, maana nasali daima dhidi ya maovu yao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Afadhali mtu mwema anipige kunionya; lakini sikubali kamwe kusifiwa na wabaya, maana nasali daima dhidi ya maovu yao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Afadhali mtu mwema anipige kunionya; lakini sikubali kamwe kusifiwa na wabaya, maana nasali daima dhidi ya maovu yao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda maovu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 141:5
23 Marejeleo ya Msalaba  

Ikawa, aliposema naye, mfalme akamwambia, Je! Tumekutia wewe kuwa mshauri wa mfalme? Nyamaza; kwa nini upigwe? Ndipo yule nabii akaacha, akasema, Najua ya kuwa Mungu amekusudia kukuangamiza, kwa sababu umeyafanya haya, wala hukulisikiliza shauri langu.


Ee BWANA, uwatendee mema walio wema, Nao walio wanyofu wa moyo.


Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.


Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako, Uzijenge kuta za Yerusalemu.


Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.


Pasipo ushauri mipango vuhunjika; Bali kwa wingi wa washauri huthibitika.


Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.


Mpige mwenye mzaha, na mjinga atapata busara; Mwonye mwenye ufahamu, naye atatambua maarifa.


Kipuli cha dhahabu, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo mwonyaji mwenye hekima kwa sikio lisikialo.


Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.


Heri kusikia laumu ya wenye hekima, Kuliko mtu kusikia wimbo wa wapumbavu;


Usimchukie ndugu yako moyoni mwako; ni lazima kumkemea jirani yako, au ulipizwe uovu kwa ajili yake


lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,


Ndugu zangu, mtu akishikwa katika kosa lolote, ninyi mlio wa Roho mrejesheni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.


Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.