Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 14:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Hapo ndipo waovu watakaposhikwa na hofu nyingi, Maana Mungu yupo pamoja na kizazi cha haki.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hapo watashikwa na hofu kubwa, maana Mungu yu pamoja na waadilifu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hapo watashikwa na hofu kubwa, maana Mungu yu pamoja na waadilifu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hapo watashikwa na hofu kubwa, maana Mungu yu pamoja na waadilifu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu, maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu, maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Hapo ndipo waovu watakaposhikwa na hofu nyingi, Maana Mungu yupo pamoja na kizazi cha haki.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 14:5
19 Marejeleo ya Msalaba  

Mfalme Ahasuero akawaambia malkia Esta na Mordekai, Myahudi, akasema, Tazama, nimekwisha kumpa Esta nyumba yake Hamani, naye mwenyewe wamekwisha kumtundika juu ya mti, kwa sababu aliwatia mikono Wayahudi.


Wazawa wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.


Wazawa wake watamtumikia. Zitasimuliwa habari za BWANA, Kwa kizazi kitakachokuja,


Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao, Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.


BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu.


Mungu yu katikati ya mji hautatetemeshwa; Mungu atausaidia asubuhi na mapema.


BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.


Hapo waliingiwa na hofu pasipokuwapo hofu, Maana Mungu ameitawanya mifupa yake aliyekuhusuru. Umewatia aibu, Kwa sababu MUNGU amewadharau.


Kama ningalisema, Nitasimulia kama hayo; Kumbe! Ningaliwadanganya kizazi cha wana wako.


Hofu na woga zimewaangukia; Kwa uweza wa mkono wako wanakaa kimya kama jiwe; Hata watakapovuka watu wako, Ee BWANA, Hata watakapovuka watu wako uliowanunua.


Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu; Bali wenye haki ni wajasiri kama simba.


Paza sauti, piga kelele, mwenyeji wa Sayuni; Maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu kati yako.


usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kulia wa haki yangu.


Fanyeni shauri pamoja, nalo litabatilika; Semeni neno, lakini halitasimama; Kwa maana Mungu yu pamoja nasi.


Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.


Bali ninyi ni uzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;


Kukawa na tetemeko katika kambi, na katika mashamba, na katikati ya watu wote; watu wa ngomeni, na watekaji nyara, wakatetemeka nao; hata na nchi ikatetemeka pia; basi kulikuwa na tetemeko kubwa mno.