Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 133:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Tazama, jinsi ilivyo vyema, na kupendeza, Ndugu kuishi pamoja, kwa umoja.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ni jambo zuri na la kupendeza sana ndugu kuishi pamoja kwa umoja.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ni jambo zuri na la kupendeza sana ndugu kuishi pamoja kwa umoja.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ni jambo zuri na la kupendeza sana ndugu kuishi pamoja kwa umoja.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Tazama jinsi ilivyo vyema na kupendeza ndugu wanapoishi pamoja katika umoja!

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Tazama jinsi ilivyo vyema na kupendeza wakati ndugu wanapoishi pamoja katika umoja!

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Tazama, jinsi ilivyo vyema, na kupendeza, Ndugu kuishi pamoja, kwa umoja.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 133:1
20 Marejeleo ya Msalaba  

Abramu akamwambia Lutu, Basi, usiwepo ugomvi, nakusihi, kati yangu na wewe, wala kati ya wachungaji wangu na wachungaji wako; maana sisi tu jamaa moja.


Akaagana na ndugu zake, wakaenda zao; naye akawaambia, Msigombane njiani.


Nilifurahi waliponiambia, Twende nyumbani kwa BWANA.


Kama si BWANA aliyekuwa pamoja nasi, Israeli na aseme sasa,


BWANA, moyo wangu hauna kiburi, Wala macho yangu hayainuki. Wala sijishughulishi na mambo makuu, Wala mambo yanayozidi nguvu zangu.


Na wivu wa Efraimu utaondoka, na wale wanaomwudhi Yuda watakatiliwa mbali; Efraimu hatamhusudu Yuda, wala Yuda hatamwudhi Efraimu.


Mbwamwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwanasimba na ng'ombe wanono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza.


Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua BWANA, kama vile maji yanavyoifunika bahari.


nami nitawapa moyo mmoja na njia moja, wapate kunicha sikuzote; kwa mema yao, na ya watoto wao baada yao;


na nyumba ikifitinika juu ya nafsi yake, nyumba hiyo haiwezi kusimama.


Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.


Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Basi ndugu, nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu migawanyiko, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja.


Upendano wa ndugu na udumu.


Neno la mwisho ni hili; muwe na nia moja, wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu;