Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 132:15 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Hakika nitavibariki vyakula vyake Wahitaji wake nitawashibisha chakula.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nitaubariki sana mji wa Siyoni kwa mahitaji yake; nitawashibisha chakula maskini wake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nitaubariki sana mji wa Siyoni kwa mahitaji yake; nitawashibisha chakula maskini wake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nitaubariki sana mji wa Siyoni kwa mahitaji yake; nitawashibisha chakula maskini wake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Hakika nitavibariki vyakula vyake Wahitaji wake nitawashibisha chakula.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 132:15
24 Marejeleo ya Msalaba  

Maana hushibisha nafsi yenye shauku, Na nafsi yenye njaa huijaza mema.


Ndiye aletaye amani mipakani mwako, Hukushibisha kwa ngano safi.


Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao BWANA watamsifu; Mioyo yenu na iishi milele.


Watashibishwa kwa unono wa nyumba yako, Nawe utawanywesha kutoka mto wa furaha zako.


Hawataaibika wakati wa ubaya, Na siku za njaa watashiba.


Umtumaini BWANA ukatende mema, Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.


Nanyi mtamtumikia BWANA, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako.


Huyu ndiye atakayekaa juu; majabali ni ngome yake; atapewa chakula chake; maji yake hayatakoma.


Nami nitaishibisha roho ya makuhani kwa unono, na watu wangu watashiba kwa wema wangu, asema BWANA.


Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamtosheki na vinywaji; mnajivika nguo lakini hampati joto; na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotobokatoboka.


Mlitazamia vingi, kumbe vikatokea vichache; tena mlipovileta nyumbani nikavipeperusha mbali. Ni kwa sababu gani? Asema BWANA wa majeshi. Ni kwa sababu yumba yangu imebaki kuwa gofu la nyumba, wakati ambapo kila mmoja wenu anakimbilia nyumbani kwake.


Kama hamtaki kusikia, na kama hamtaki kuitia moyoni, ili kulitukuza jina langu, asema BWANA wa majeshi, basi nitawaleteeni laana, nami nitazilaani baraka zenu; naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamyatii haya moyoni.


Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.


Wenye njaa amewashibisha mema, Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.


na Mlawi kwa kuwa hana fungu wala urithi pamoja nawe, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako, na waje wale na kushiba; ili kwamba BWANA, Mungu wako, akubarikie katika kazi yote ya mkono wako uifanyayo.