Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 13:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nitakuwa na wasiwasi rohoni mwangu hadi lini, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Adui yangu atatukuka juu yangu hadi lini?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nitakuwa na wasiwasi rohoni hadi lini, na sikitiko moyoni siku hata siku? Hadi lini adui zangu watafurahia taabu zangu?

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nitakuwa na wasiwasi rohoni hadi lini, na sikitiko moyoni siku hata siku? Hadi lini adui zangu watafurahia taabu zangu?

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nitakuwa na wasiwasi rohoni hadi lini, na sikitiko moyoni siku hata siku? Hadi lini adui zangu watafurahia taabu zangu?

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nitapambana na mawazo yangu hadi lini, na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu? Adui zangu watanishinda hadi lini?

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini, na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu? Adui zangu watanishinda mpaka lini?

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nitakuwa na wasiwasi rohoni mwangu hadi lini, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Adui yangu atatukuka juu yangu hadi lini?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 13:2
44 Marejeleo ya Msalaba  

Basi mfalme akaniambia, Mbona umesikitika uso wako, nawe huna ugonjwa? Nini hii, isipokuwa ni huzuni ya moyo? Ndipo nikaogopa sana.


Esta akasema, Ni mtesi, tena ni adui, ndiye huyu Hamani, mtu mbaya kabisa. Mara Hamani akaingiwa na hofu mbele ya mfalme na malkia.


Mimi nikiwa mwovu, ole wangu! Nami nikiwa mwenye haki, walakini sitainua kichwa changu; Maana nimejaa aibu Nikiyaangalia mateso yangu.


Ili kumhukumu yatima na aliyeonewa, Binadamu aliye udongo asizidi kudhulumu.


Kamba za mauti zilinizunguka, Shida za kuzimu zilinipata. Nilipata dhiki na mateso;


Wasinione wasio haki wanaonionea, Adui za roho yangu wanaonizunguka.


Midomo ya uongo iwe na ububu, Imneneayo mwenye haki maneno ya kiburi, Kwa majivuno na dharau.


Kwa maana mimi ni karibu na kusita, Na maumivu yangu yako mbele yangu daima.


Nayakumbuka mambo haya kwa uchungu moyoni mwangu, Jinsi nilivyokuwa nikienda na mkutano, Na kuwaongoza hadi katika nyumba ya Mungu, Kwa sauti ya furaha na kusifu, mkutano wa sikukuu.


BWANA urudi, uniopoe nafsi yangu, Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.


Asije akaipapura nafsi yangu kama simba, Akaniburura hadi pasipokuwa na wa kuniponya.


Ee Mungu, mtesi atalaumu hata lini? Adui alidharau jina lako hata milele?


Ee BWANA, uyakumbuke hayo, adui amelaumu, Na watu wapumbavu wamelidharau jina lako.


Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu; Kwa sababu yao wanaoshindana nawe; Uwakomeshe adui na mjilipiza kisasi.


Adui wameangamia na kuwa magofu milele. Nayo miji yao uliing'oa; Hata kumbukumbu lao limepotea.


Moyo wa furaha huchangamsha uso; Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.


Siku zake zote hula gizani, mwenye fadhaa nyingi, mwenye ugonjwa na uchungu.


Mbona maumivu yangu ni ya daima, na jeraha langu halina dawa, linakataa kuponywa? Je! Yamkini wewe utakuwa kwangu kama kijito kidanganyacho, na kama maji yasiyodumu?


Ulisema, Ole wangu! Kwa maana BWANA ameongeza huzuni pamoja na maumivu yangu. Nimechoka kwa ajili ya kuugua kwangu, wala sioni raha.


Laiti ningeweza kujifariji, nisione huzuni! Moyo wangu umezimia ndani yangu.


Watesi wake wamekuwa kichwa, Adui zake hufanikiwa; Kwa kuwa BWANA amemtesa Kwa sababu ya wingi wa makosa yake; Watoto wake wadogo wamechukuliwa mateka Mbele yake huyo mtesi.


Uchafu wake ulikuwa katika marinda yake; Hakukumbuka mwisho wake; Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu; Yeye hana mtu wa kumfariji; Tazama, BWANA, mateso yangu; Maana huyo adui amejitukuza.


Mbona watusahau sikuzote; Na kutuacha muda huu mwingi?


Ndipo akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami.


Kila siku nilipokuwa pamoja nanyi hekaluni hamkuninyoshea mikono, lakini hii ndiyo saa yenu, na mamlaka ya giza.


Ila kwa sababu nimewaambia hayo huzuni imejaa mioyoni mwenu.


ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyoisha moyoni mwangu.


Kwa maana alikuwa mgonjwa sana, karibu kufa; lakini Mungu alimhurumia; wala si yeye peke yake, ila na mimi pia; nisiwe na huzuni juu ya huzuni.


Naye Sauli akazidi kumwogopa Daudi; tangu wakati huo, Sauli akawa adui yake Daudi daima.


Maana mtu akimwona adui yake, je! Atamwacha aende zake salama? Basi BWANA na akulipe mema kwa haya uliyonitendea leo.