Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 129:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Na waaibishwe, warudishwe nyuma, Wote wanaoichukia Sayuni.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Na waaibishwe na kurudishwa nyuma, wote wale wanaouchukia mji wa Siyoni.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Na waaibishwe na kurudishwa nyuma, wote wale wanaouchukia mji wa Siyoni.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Na waaibishwe na kurudishwa nyuma, wote wale wanaouchukia mji wa Siyoni.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wale wote wanaoichukia Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na waaibishwe, warudishwe nyuma, Wote wanaoichukia Sayuni.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 129:5
17 Marejeleo ya Msalaba  

Ikawa adui zetu wote waliposikia, ndipo wamataifa wote waliotuzunguka wakaogopa, nao wakakata tamaa sana machoni pao wenyewe; maana waliitambua kazi hiyo ilivyotendwa na Mungu wetu.


Basi Hamani akawasimulia Zereshi mkewe na marafiki zake wote kila neno lililompata. Kisha watu wake wenye hekima na Zereshi mkewe wakamwambia, Ikiwa huyu Mordekai, ambaye umeanza kuanguka mbele yake, ni wa uzao wa Wayahudi, wewe hutamweza, bali kuanguka utaanguka mbele yake.


Basi Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na kuwachinja, na kuwaangamiza, wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia.


Uombeeni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao;


Wafadhaike kwa aibu yao, Wanaoniambia Ewe! Ewe!


Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu. Wavikwe laumu na aibu wanaonitakia mabaya.


Basi, itakuwa, Bwana atakapokuwa ameitimiza kazi yake yote juu ya mlima Sayuni na juu ya Yerusalemu, nitamwadhibu matunda ya kiburi cha moyo wake mfalme wa Ashuru, na majivuno ya macho yake.


Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni.


tamko alilolitamka BWANA katika habari zake ndilo hili; Bikira, binti Sayuni, anakudharau, anakudhihaki sana; binti Yerusalemu anatikisa kichwa chake juu yako.


Nami nitaulinda mji huu, niuokoe kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi, mtumishi wangu.


Na sasa mataifa mengi wamekusanyika juu yako, wasemao, Na atiwe unajisi; macho yetu na yaone shari ya Sayuni.


Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata majeraha mengi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake.


Siku hiyo nitawafanya wakuu wa Yuda kuwa kama kigae chenye moto katika kuni, na kama kinga cha moto katika miganda; nao watateketeza watu wa kila kabila, wawazungukao pande zote, upande wa mkono wa kulia na upande wa mkono wa kushoto; na baada ya haya Yerusalemu utakaa mahali pake, naam, hapo Yerusalemu.


Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maranatha.