Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 129:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

BWANA ndiye mwenye haki, Amezikata kamba zao wasio haki.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini Mwenyezi-Mungu ni mwadilifu; amezikata kamba za hao watu waovu.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini Mwenyezi-Mungu ni mwadilifu; amezikata kamba za hao watu waovu.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini Mwenyezi-Mungu ni mwadilifu; amezikata kamba za hao watu waovu.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini Mwenyezi Mungu ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

BWANA ndiye mwenye haki, Amezikata kamba zao wasio haki.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 129:4
9 Marejeleo ya Msalaba  

Ee BWANA, Mungu wa Israeli, wewe ndiwe mwenye haki, maana sisi tumesalia, mabaki yaliyookoka, kama hivi leo; tazama, sisi tupo hapa wenye hatia mbele zako; maana hapana mtu awezaye kusimama mbele zako kwa sababu ya jambo hili.


Lakini wewe u mwenye haki, katika hayo yote yaliyotupata; maana wewe umetenda yaliyo kweli, lakini sisi tumetenda yaliyo maovu;


Ee BWANA, Wewe ndiwe mwenye haki, Na hukumu zako ni za adili.


Mtu asipoongoka ataunoa upanga wake; Ameupinda uta wake na kuuweka tayari;


BWANA ndiye mwenye haki; Maana nimeiasi amri yake; Sikieni, nawasihi, enyi watu wote, Mkayatazame majonzi yangu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wamechukuliwa mateka.


Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.


Ee Bwana, haki ina wewe, lakini kwetu sisi kuna aibu, kama hivi leo; kwa watu wa Yuda, na kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa Israeli wote, walio karibu na hao walio mbali, katika nchi zote ulikowafukuza, kwa sababu ya makosa yao waliyokukosa.