Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 124:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Papo hapo wangalitumeza hai, Hasira yao ilipowaka juu yetu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

hakika tungalimezwa tukiwa hai, wakati hasira zao zilipotuwakia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

hakika tungalimezwa tukiwa hai, wakati hasira zao zilipotuwakia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

hakika tungalimezwa tukiwa hai, wakati hasira zao zilipotuwakia.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangetumeza tukiwa hai,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Papo hapo wangalitumeza hai, Hasira yao ilipowaka juu yetu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 124:3
18 Marejeleo ya Msalaba  

Akaona haitoshi kumtia mikono Mordekai peke yake; maana wamemjulisha kabila lake Mordekai; kwa hiyo Hamani alitaka kuwaangamiza Wayahudi wote waliokuwa wakikaa katika ufalme wote mzima wa Ahasuero, yaani, watu wake Mordekai.


Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka.


Wasiseme moyoni, Haya! Ndivyo tutakavyo; Wasiseme, Tumemmeza.


Atanitumia msaada toka mbinguni na kuniokoa, Atawaaibisha wale wanaotaka kunishambulia. Mungu atazituma Fadhili zake na kweli yake.


Walisema mioyoni mwao, Na tuwaangamize kabisa; Mahali penye mikutano ya Mungu Wamepachoma moto katika nchi pia.


Maana hasira ya binadamu itakusifu, Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.


Wamesema, Njoni, tuwakatilie mbali wasiwe taifa, Na jina la Israeli halitakumbukwa tena.


Maana wanashauriana kwa moyo mmoja, Juu yako wanafanyana agano.


Tuwameze hai kama kuzimu, Na wazima, kama wao washukao shimoni.


Nebukadneza, mfalme wa Babeli, amenila, ameniponda, amenifanya kuwa chombo kitupu; amenimeza kama joka, amelijaza tumbo lake vitu vyangu vya anasa; amenitupa


Ndipo Nebukadneza akajaa ghadhabu, na sura ya uso wake ikabadilika juu ya Shadraka, na Meshaki, na Abednego, basi akatoa amri watie moto ile tanuri mara saba kuliko desturi yake ya kutiwa moto.


BWANA akaweka tayari samaki mkubwa ili ammeze Yona, naye Yona akawa ndani ya tumbo la samaki yule muda wa siku tatu, mchana na usiku.


Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale majusi, alighadhibika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wa kiume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake kote, kuanzia wenye miaka miwili na chini yake, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale majusi.


akataka ampe barua za kuenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, wanaume kwa wanawake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu.