Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 121:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwenyezi-Mungu atakulinda katika shughuli zako zote tangu sasa na hata milele.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwenyezi-Mungu atakulinda katika shughuli zako zote tangu sasa na hata milele.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenyezi-Mungu atakulinda katika shughuli zako zote tangu sasa na hata milele.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mwenyezi Mungu atakulinda unapoingia na unapotoka, tangu sasa na hata milele.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

bwana atakulinda unapoingia na unapotoka, tangu sasa na hata milele.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

BWANA atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 121:8
12 Marejeleo ya Msalaba  

Zamani za kale, hapo Sauli alipokuwa mfalme juu yetu, wewe ndiwe uliyewaongoza Israeli wakitoka nje kwenda, na kurudi vitani. Naye BWANA akakuambia, Wewe utawalisha watu wangu Israeli, nawe utakuwa mkuu juu ya Israeli.


Ndipo nikaamuru kufunga, hapo penye mto Ahava, ili tupate kujinyenyekeza mbele za Mungu, na kutafuta kwake njia iliyonyoka, kwa ajili yetu sisi wenyewe, na kwa ajili ya watoto wetu, na kwa mali yetu yote.


Ndipo tukasafiri toka mtoni Ahava siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza, ili kwenda Yerusalemu; na mkono wa Mungu ulikuwa pamoja nasi, akatuokoa na mkono wa adui, na mtu mwenye kutuvizia njiani.


Jina la BWANA lihimidiwe Tangu leo na hata milele.


Bali sisi tutamhimidi BWANA, Tangu leo na hata milele.


Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo BWANA anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele.


Ee Israeli, umtarajie BWANA, Tangu leo na hata milele.


Apate kuyalinda mapito ya hukumu, Na kuhifadhi njia ya watakatifu wake.


Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.


Utalaaniwa uingiapo, utalaaniwa na utokapo,


Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo.