Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 112:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Heri atendaye fadhili na kukopesha; Atengenezaye mambo yake kwa haki.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mtu mkarimu akopeshaye bila faida, hufanikiwa; mtu afanyaye shughuli zake kwa kutumia haki.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mtu mkarimu akopeshaye bila faida, hufanikiwa; mtu afanyaye shughuli zake kwa kutumia haki.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mtu mkarimu akopeshaye bila faida, hufanikiwa; mtu afanyaye shughuli zake kwa kutumia haki.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Heri atendaye fadhili na kukopesha; Atengenezaye mambo yake kwa haki.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 112:5
22 Marejeleo ya Msalaba  

Basi, nikaweka watu, mahali pa chini pa nafasi iliyokuwa nyuma ya ukuta, mahali palipokuwa wazi, kwa kadiri ya jamaa zao, nikawaweka waliojihami na panga zao, na mikuki yao, na pinde zao.


Asiye haki hukopa wala halipi, Bali mwenye haki hufadhili, hukirimu.


Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA; Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.


Asiye na hekima hupeana mkono na mtu; Na kuwa mdhamini wa mtu mwingine.


Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharibifu.


Ili upate kwenda katika njia ya watu wema, Na kuyashika mapito ya wenye haki.


Tengeneza kazi yako huko nje, Jifanyizie kazi yako tayari shambani, Ukiisha, jenga nyumba yako.


Na tazama, akatoka mtu mmoja, jina lake Yusufu, ambaye ni mtu wa baraza, mtu mwema, mwenye haki;


Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo, na thawabu yenu itakuwa nyingi; nanyi mtakuwa wana wa Aliye Juu, kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasiomshukuru, na waovu.


Nao waliposhiba, aliwaambia wanafunzi wake, Kusanyeni vipande vilivyobaki, kisipotee chochote.


Maana alikuwa mtu mwema amejaa Roho Mtakatifu na imani; watu wengi wakaongezeka upande wa Bwana.


kwa bidii, bila kulegea; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;


Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema.


Basi angalieni sana jinsi mnavyoenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;


Na hii ndiyo dua yangu, kwamba pendo lenu lizidi kuwa jingi sana, katika hekima na ufahamu wote;


Nendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati.