Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 109:27 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nao wakajue ya kuwa huu ni mkono wako; Wewe, BWANA, umeyafanya hayo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Waoneshe watu kuwa ndiwe uliyetenda hayo, wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ndiwe uliyefanya hivyo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Waoneshe watu kuwa ndiwe uliyetenda hayo, wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ndiwe uliyefanya hivyo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Waoneshe watu kuwa ndiwe uliyetenda hayo, wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ndiwe uliyefanya hivyo.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Mwenyezi Mungu, umetenda hili.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee bwana, umetenda hili.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nao wakajue ya kuwa huu ni mkono wako; Wewe, BWANA, umeyafanya hayo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 109:27
12 Marejeleo ya Msalaba  

huyo Ezra akakwea kutoka Babeli; naye alikuwa mwandishi mwepesi katika Sheria ya Musa, aliyokuwa ameitoa BWANA, Mungu wa Israeli; naye mfalme akamjalia matakwa yake yote, kama mkono wa BWANA, Mungu wake, ulivyokuwa pamoja naye.


Ikawa adui zetu wote waliposikia, ndipo wamataifa wote waliotuzunguka wakaogopa, nao wakakata tamaa sana machoni pao wenyewe; maana waliitambua kazi hiyo ilivyotendwa na Mungu wetu.


Huufunga mkono wa kila binadamu; Ili watu wote aliowaumba wajue.


Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko, Na ulimi wetu kelele za furaha. Ndipo waliposema katika mataifa, BWANA amewatendea mambo makuu.


Ndipo wale waganga wakamwambia Farao, Jambo hili ni kidole cha Mungu; na moyo wake Farao ukawa mgumu asiwasikize; vile vile kama BWANA alivyonena.


wakisema, Tuwafanyie nini watu hawa? Maana ni dhahiri kwa watu wote wakaao Yerusalemu ya kwamba ishara mashuhuri imefanywa nao, wala hatuwezi kuikana.