Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 106:36 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Wakazitumikia sanamu zao, Nazo zikawa mtego kwao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Waliabudu sanamu za miungu yao, nazo zikawa mtego wa kuwaangamiza.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Waliabudu sanamu za miungu yao, nazo zikawa mtego wa kuwaangamiza.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Waliabudu sanamu za miungu yao, nazo zikawa mtego wa kuwaangamiza.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wakazitumikia sanamu zao, Nazo zikawa mtego kwao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 106:36
18 Marejeleo ya Msalaba  

Yalitukia hayo kwa sababu wana wa Israeli walikuwa wametenda dhambi juu ya BWANA, Mungu wao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri watoke chini ya mkono wa Farao mfalme wa Misri, wakawaacha miungu mingine.


Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu, Wakamtia wivu kwa sanamu zao.


Wasikae katika nchi yako, wasije wakakufanya kunitendea mimi dhambi; kwa sababu ukiitumikia miungu yao, jambo hili halikosi litakuwa ni (mtego) tanzi kwako.


Ndipo watakaposema watu, Ni kwa kuwa waliacha agano la BWANA, Mungu wa baba zao, alilofanya nao hapo alipowatoa katika nchi ya Misri;


Nawe angamiza mataifa yote atakayokupa BWANA, Mungu wako; jicho lako lisiwahurumie, wala usiitumikie miungu yao; kwani jambo hilo litakuwa ni mtego kwako.


jueni hakika ya kuwa BWANA, Mungu wenu, hatawafukuza tena mataifa haya mbele ya macho yenu, bali watakuwa mtego kwenu na tanzi, na mjeledi mbavuni mwenu, na miiba machoni mwenu, hadi mtakapoangamia na kutoka katika nchi hii njema, ambayo BWANA, Mungu wenu, amewapa ninyi.


Kisha wana wa Israeli walifanya tena yaliyo maovu mbele za macho ya BWANA, wakawatumikia Mabaali, na Maashtorethi, na miungu ya Shamu, na miungu ya Sidoni, na miungu ya Moabu, na miungu ya wana wa Amoni, na miungu ya Wafilisti; nao wakamuacha BWANA, wala hawakumtumikia yeye.


Lakini hawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine, wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za BWANA bali wao hawakufanya hivyo.


Lakini ikawa, wakati alipokufa mwamuzi huyo, wakarudi nyuma wakafanya maovu kuliko baba zao, kwa kuifuata miungu mingine ili kuitumikia, na kuinama mbele yao; hawakuacha matendo yao, wala njia zao za ukaidi.


Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni mtego kwenu.