Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 106:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya BWANA, Au kuzihubiri sifa zake zote?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ni nani awezaye kutaja matendo ya Mwenyezi-Mungu? Ni nani awezaye kumsifu kama anavyostahili?

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ni nani awezaye kutaja matendo ya Mwenyezi-Mungu? Ni nani awezaye kumsifu kama anavyostahili?

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ni nani awezaye kutaja matendo ya Mwenyezi-Mungu? Ni nani awezaye kumsifu kama anavyostahili?

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Mwenyezi Mungu au kutangaza kikamilifu sifa zake?

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya BWANA, Au kuzihubiri sifa zake zote?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 106:2
9 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo Walawi, Yeshua na Kadmieli, na Bani, na Hashabneya, na Sherebia, na Hodia, na Shebania, na Pethahia, wakasema, Simameni, mkamhimidi BWANA, Mungu wenu, tangu milele na hata milele. Na lihimidiwe jina lako tukufu, lililotukuka kuliko baraka zote na sifa zote.


Tazama, hivi ni viunga tu vya njia zake; Na jinsi yalivyo madogo manong'ono tusikiayo katika habari zake! Lakini ngurumo za uweza wake ni nani awezaye kuzielewa?


Yeye afanyaye mambo makuu, yasiyotambulikana; Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu;


Ee BWANA, Mungu wangu, umefanya kwa wingi Miujiza yako na mawazo yako kwetu; Hakuna awezaye kufananishwa nawe; Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri, Ni mengi sana hayahesabiki.


Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazieleweki!


na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake;


ili mpate kufahamu pamoja na watakatifu wote jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina;