Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 105:15 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Msiwaguse wateule wangu; msiwadhuru manabii wangu!”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Msiwaguse wateule wangu; msiwadhuru manabii wangu!”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Msiwaguse wateule wangu; msiwadhuru manabii wangu!”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Msiwaguse niliowapaka mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 105:15
14 Marejeleo ya Msalaba  

Basi sasa umrudishe mwanamke kwa mtu huyo, maana yeye ni nabii, naye atakuombea, upate kuishi. Bali usipomrudisha, fahamu ya kwamba kwa hakika utakufa wewe na watu wote ulio nao.


Basi Abimeleki akawaamuru watu wote, akisema, Amgusaye mtu huyu au mkewe lazima atauawa.


Daudi akamwambia, Jinsi gani hukuogopa kuunyosha mkono wako umwangamize masihi wa BWANA?


Ikawa, mfalme Yeroboamu alipoyasikia maneno ya yule mtu wa Mungu, alipopiga kelele juu ya madhabahu huko Betheli, alinyosha mkono wake pale madhabahuni, akasema, Mkamateni. Basi ule mkono wake aliounyosha ukakatika, wala hakuweza kuurudisha kwake tena.


Na Yehu mwana wa Nimshi mtie mafuta awe mfalme wa Israeli; na Elisha mwana wa Shafati wa Abel-Mehola mtie mafuta awe nabii mahali pako.


Basi Hamani akawasimulia Zereshi mkewe na marafiki zake wote kila neno lililompata. Kisha watu wake wenye hekima na Zereshi mkewe wakamwambia, Ikiwa huyu Mordekai, ambaye umeanza kuanguka mbele yake, ni wa uzao wa Wayahudi, wewe hutamweza, bali kuanguka utaanguka mbele yake.


Mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, na Seraya, mwana wa Azrieli, na Shelemia, mwana wa Abdeeli, wamkamate Baruku, mwandishi, na Yeremia, nabii; lakini BWANA aliwaficha.


Mtwae, umtunze sana, wala usimtende neno baya lolote; lakini umtendee kama atakavyokuambia.


Na BWANA atairithi Yuda, iwe sehemu yake katika nchi takatifu, naye atachagua Yerusalemu tena.


Kwa maana BWANA wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake.


Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake.