Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 102:17 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, Asiyadharau maombi yao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ataikubali sala ya fukara; wala hatayakataa maombi yao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ataikubali sala ya fukara; wala hatayakataa maombi yao.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ataikubali sala ya fukara; wala hatayakataa maombi yao.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, Asiyadharau maombi yao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 102:17
16 Marejeleo ya Msalaba  

Ee Bwana, nakusihi, litege sikio lako, uyasikilize maombi ya mtumishi wako, na maombi ya watumishi wako, wanaofurahi kulicha jina lako; nakuomba sana; unifanikishe mimi, mtumishi wako, leo, ukanijalie rehema mbele ya mtu huyu. (Maana, nilikuwa mnyweshaji wa mfalme).


tega sikio lako, macho yako yakafumbuke, upate kuyasikiliza maombi ya mtumishi wako, ninayoomba mbele zako wakati huu, mchana na usiku, kwa ajili ya wana wa Israeli, watumishi wako; hapo ninapoziungama dhambi za wana wa Israeli, tulizozifanya juu yako; naam, mimi na nyumba ya baba yangu tumefanya dhambi.


Ndipo nikawajibu, nikawaambia, Mungu wa mbinguni, yeye atatufanikisha; kwa hiyo sisi, watumishi wake, tutaondoka na kujenga; lakini ninyi hamna sehemu, wala haki, wala kumbukumbu, katika Yerusalemu.


BWANA ndiye aijengaye Yerusalemu, Huwakusanya waliotawanyika wa Israeli.


Maana hapuuzi Wala kuchukizwa na mateso ya anayeteswa, Wala hamfichi uso wake, Bali humsikia akimlilia.


Macho yao yatiwe giza wasione, Na viuno vyao uvitetemeshe daima.


Kwa maana atamkomboa mhitaji aliapo, Na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi.


Kwa maana mhitaji hatasahauliwa daima; Matumaini ya wanyonge hayatapotea milele.


Na utukufu wa BWANA utafunuliwa, Na watu wote watauona pamoja; Kwa kuwa kinywa cha BWANA kimenena haya.


nilithibitishaye neno la mtumishi wangu, na kuyafikiliza mashauri ya wajumbe wangu; niuambiaye Yerusalemu, Utakaliwa na watu, nayo miji ya Yuda, Itajengwa, nami nitapainua mahali pake palipobomoka;


Tazama, siku zinakuja, asema BWANA, mji huu utakapojengwa kwa ajili ya BWANA, toka mnara wa Hananeli hadi katika lango la pembeni.


Kwa kuwa BWANA atawaamua watu wake, Atawahurumia watumwa wake, Aonapo ya kuwa nguvu zao zimeondoka, Na ya kuwa habaki mtu, aliyefungwa wala asiyefungwa,


Lakini huko, kama mkimtafuta BWANA, Mungu wako, utampata, ukimtafuta kwa moyo wako wote, na roho yako yote.