Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 10:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kinywa chake kimejaa laana, Na hila na dhuluma. Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu,

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kinywa chake kimejaa laana, udanganyifu na dhuluma; mwepesi kusema maneno ya kuchukiza na maovu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kinywa chake kimejaa laana, udanganyifu na dhuluma; mwepesi kusema maneno ya kuchukiza na maovu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kinywa chake kimejaa laana, udanganyifu na dhuluma; mwepesi kusema maneno ya kuchukiza na maovu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kinywa chake kimejaa laana, uongo na vitisho; shida na ubaya viko chini ya ulimi wake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kinywa chake kimejaa laana, uongo na vitisho; shida na ubaya viko chini ya ulimi wake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kinywa chake kimejaa laana, Na hila na dhuluma. Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu,

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 10:7
29 Marejeleo ya Msalaba  

Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Na mioyo yao hutunga udanganyifu.


Ingawa uovu ni mtamu kinywani mwake, Ingawa auficha chini ya ulimi wake;


Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe, Wenye midomo ya kujipendekeza; Husemezana kwa mioyo ya unafiki;


Wamenoa ndimi zao na kuwa kama za nyoka, Na katika midomo yao mna sumu ya fira.


Nao wainuapo vichwa watu wanaonizunguka, Madhara ya midomo yao yawafunike.


Uniponye, unitoe, Katika mkono wa wageni. Vinywa vyao vyasema visivyofaa, Na mkono wao wa kulia ni mkono wa uongo.


Vinywa vyao vinasema visivyofaa, Na ambao mikono yao ya kulia ni ya uongo.


Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila, Ameacha kuwa na akili na kutenda mema.


Na mmoja wao akija kunitazama asema uongo, Moyo wake hujikusanyia maovu, Naye atokapo nje huyanena.


Maana vinywani mwao hamna uaminifu; Moyo wao ni shimo tupu, koo lao ni kaburi wazi, Ulimi wao hujipendekeza.


Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, Na ulimi wako unatunga uongo.


Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila.


Kinywa chake ni laini kuliko siagi, Bali moyo wake ni vita. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, Lakini yanakata kama upanga mkali.


Waovu hupotoka hata kabla ya kuzaliwa kwao; Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.


Kwa dhambi ya kinywa chao, Na kwa neno la midomo yao, Wanaswe kwa kiburi chao, Kwa ajili ya kulaani na uongo wasemao.


Uwakomeshe kwa hasira, Uwakomeshe watoweke, Wajue ya kuwa Mungu atawala katika Yakobo, Na hata miisho ya dunia.


Mpango wao ni kumwangusha tu mtu mwenye cheo; Huufurahia uongo. Kwa kinywa chao hubariki; Kwa moyo wao hulaani.


Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wanaoyalenga maneno ya uchungu kama mishale,


Tazama, huyu ametunga uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.


Hudhihaki, husimulia mabaya, Husimulia udhalimu kana kwamba wako juu.


Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongo Ni moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.


Uniondolee ubatili na uongo; Usinipe umaskini wala utajiri; Unilishe chakula kilicho kadiri yangu.


Hakuna anayeshitaki kwa haki, wala hapana atetaye kwa kweli; hutumainia ubatili, hunena uongo; hupata mimba ya madhara, na kuzaa uovu.


Huupinda ulimi wao, kana kwamba ni upinde, ili kusema uongo; nao wamepata nguvu katika nchi, lakini si katika uaminifu; maana huendelea toka ubaya hata ubaya, wala hawanijui mimi, asema BWANA.


Makao yako ya katikati ya hadaa; kwa hadaa wanakataa kunijua mimi, asema BWANA.


Lisikieni hili, ninyi mnaopenda kuwameza wahitaji, na kuwakomesha maskini wa nchi,


Enyi wazawa wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.