Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yohana 5:38 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Wala neno lake hamnalo likikaa ndani yenu, kwa kuwa ninyi hammwamini yule aliyetumwa na yeye.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

na ujumbe wake haukai ndani yenu maana hamkumwamini yule aliyemtuma.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

na ujumbe wake haukai ndani yenu maana hamkumwamini yule aliyemtuma.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

na ujumbe wake haukai ndani yenu maana hamkumwamini yule aliyemtuma.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

wala hamna neno lake ndani yenu, kwa sababu hamkumwamini yeye aliyetumwa naye.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

wala hamna neno lake ndani yenu, kwa sababu hamkumwamini yeye aliyetumwa naye.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wala neno lake hamnalo likikaa ndani yenu, kwa kuwa ninyi hammwamini yule aliyetumwa na yeye.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yohana 5:38
19 Marejeleo ya Msalaba  

Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.


Mtu mbaya ajapofadhiliwa, Hata hivyo hatajifunza haki; Katika nchi ya unyofu atatenda udhalimu, Wala hatauona utukufu wa BWANA.


BWANA, mkombozi wa Israeli, Mtakatifu wake, amwambia hivi yeye anayedharauliwa na wanadamu; yeye anayechukiwa na taifa hili; yeye aliye mtumishi wao watawalao; Wafalme wataona, watasimama; wakuu nao watasujudu; kwa sababu ya BWANA aliye mwaminifu, Mtakatifu wa Israeli aliyekuchagua.


Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.


Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni lolote mtakalo nanyi mtatendewa.


Najua ya kuwa ninyi ni uzao wa Abrahamu lakini mnatafuta kuniua kwa sababu neno langu halimo ndani yenu.


Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.


Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda kulingana na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.


Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.