Yobu 6:27 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Naam, mwapenda kuwapigia kura hao mayatima, Na kufanya biashara ya rafiki yenu. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Nyinyi mnathubutu hata kuwapigia yatima kura; mnawapigia bei hata marafiki zenu! Biblia Habari Njema - BHND Nyinyi mnathubutu hata kuwapigia yatima kura; mnawapigia bei hata marafiki zenu! Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Nyinyi mnathubutu hata kuwapigia yatima kura; mnawapigia bei hata marafiki zenu! Neno: Bibilia Takatifu Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali. Neno: Maandiko Matakatifu Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali. BIBLIA KISWAHILI Naam, mwapenda kuwapigia kura hao mayatima, Na kufanya biashara ya rafiki yenu. |
Kwa sababu nilimwokoa maskini aliyenililia; Yatima naye, na yule asiyekuwa na mtu wa kumsaidia.
Wameweka wavu ili kuninasa miguu; Nimevunjika moyo; Wamechimba shimo njiani mwangu; Lakini wao wenyewe wametumbukia humo!
Usimwonee mgeni, wala kumtendea jeuri; kwa kuwa ninyi mlikuwa wageni katika nchi ya Misri.
Je! Mabaya yalipwe badala ya mema? Maana wameichimbia nafsi yangu shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele zako, ili niseme mema kwa ajili yao, nikaigeuze ghadhabu yako isiwapate.
Kilio na kisikiwe kitokacho katika nyumba zao, hapo utakapoleta kikosi juu yao kwa ghafla; kwa maana wamenichimbia shimo waninase, nao wameifichia miguu yangu mitego.
Ndani yako wamedharau baba na mama; kati yako wamewatenda wageni udhalimu; ndani yako wamewaonea yatima na mjane.
Nao wamewapigia kura watu wangu; na mvulana wamemwuza ili kupata kahaba, na msichana wamemwuza ili kupata divai, wapate kunywa.
Hata hivyo alichukuliwa mbali, alikwenda utumwani; watoto wake wachanga walisetwa kwenye maachano ya njia kuu zote; watu wake wenye heshima wakapigiwa kura, na wakuu wake wote wakafungwa kwa minyororo.
Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami sitasita kutoa ushahidi juu ya wachawi; na juu ya wazinzi, na juu ya waapao kwa uongo; juu ya wamwoneao mwajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema BWANA wa majeshi.
Dini iliyo safi, isiyo na dosari mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Na kwa tamaa yao watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa; wao ambao hukumu yao tangu zamani haikawii, wala maangamizi yao hayasinzii.