Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 6:15 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ndugu zangu wametenda udanganyifu kama kijito cha maji. Mfano wa fumbi la vijito vipitavyo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Rafiki zangu wamenidanganya kama kijito, wamenihadaa kama mitaro isiyo na maji.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Rafiki zangu wamenidanganya kama kijito, wamenihadaa kama mitaro isiyo na maji.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Rafiki zangu wamenidanganya kama kijito, wamenihadaa kama mitaro isiyo na maji.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ndugu zangu wametenda udanganyifu kama kijito cha maji. Mfano wa fumbi la vijito vipitavyo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 6:15
20 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa kuwa utasahau mateso yako; Utayakumbuka kama maji yaliyokwisha pita;


Lakini ninyi hubuni maneno ya uongo, Ninyi nyote ni matabibu wasiofaa.


Kama vile maji kupwa katika bahari, Na mto kupunguka na kukatika;


Amewaweka ndugu zangu mbali nami, Na wanijuao wametengwa nami kabisa.


Marafiki zangu wote wa dhati wanichukia; Na hao niliowapenda wamenigeukia.


Vilivyokuwa vyeusi kwa sababu ya barafu, Ambamo theluji hujificha.


Wanipendao na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu; Na jamaa zangu wanasimama mbali.


Hata rafiki yangu mwandani niliyemtumaini, Aliyekula pamoja nami, Ameniinulia kisigino chake.


Mpenzi na rafiki umewatenga nami, Nao wanijuao wamo gizani.


Kumtumaini asiye mwaminifu wakati wa taabu Ni kama jino lililovunjika, au mguu ulioteguka.


Kwa maana hata ndugu zako, na nyumba ya baba yako, wamekutenda mambo ya hila; naam, wamepiga kelele nyuma yako; usiwasadiki, wajapokuambia maneno mazuri.


Mbona maumivu yangu ni ya daima, na jeraha langu halina dawa, linakataa kuponywa? Je! Yamkini wewe utakuwa kwangu kama kijito kidanganyacho, na kama maji yasiyodumu?


Wote wakupendao wamekusahau; hawakutafuti; maana nimekujeruhi kwa jeraha la adui, kwa adhabu ya mtu mkatili; kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zilikuwa zimeongezeka.


Tazama, wanawake wote, walioachwa ndani ya nyumba ya mfalme wa Yuda, watatolewa na kuchukuliwa kwa wakuu wa mfalme wa Babeli, na wanawake hao watasema, Rafiki zako walio karibu wamekudanganya, nao wamekushinda; na kwa kuwa miguu yako imezama matopeni sasa, wamegeuka na kurudi nyuma.


Sisemi habari za ninyi nyote; nawajua wale niliowachagua; lakini andiko lipate kutimizwa, Aliyekula chakula changu Ameniinulia kisigino chake.


Tazama, saa inakuja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanyika kila mmoja kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu; lakini mimi siko peke yangu, kwa kuwa Baba yupo pamoja nami.


Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung'olewa kabisa;