Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yobu 6:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kwake huyo atakaye kuzima roho inapasa atendewe mema na rafiki; Hata kwake huyo aachaye kumcha Mwenyezi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Anayekataa kumhurumia rafiki yake, anakataa kumcha Mungu mwenye nguvu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Anayekataa kumhurumia rafiki yake, anakataa kumcha Mungu mwenye nguvu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Anayekataa kumhurumia rafiki yake, anakataa kumcha Mungu mwenye nguvu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata akiacha uchaji wa Mwenyezi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwake huyo atakaye kuzima roho inapasa atendewe mema na rafiki; Hata kwake huyo aachaye kumcha Mwenyezi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yobu 6:14
16 Marejeleo ya Msalaba  

Abrahamu akasema, Kwa kuwa niliona, hakika hapana hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa ajili ya mke wangu.


Basi ilikuwa, hapo hizo siku za karamu zao zilipokuwa zimetimia, Ayubu hutuma kwao akawatakasa, kisha akaamka asubuhi na mapema, na kusongeza sadaka za kuteketezwa kama hesabu yao wote ilivyokuwa; kwani Ayubu alisema, Pengine hawa wanangu wamefanya dhambi, na kumkufuru Mungu mioyoni mwao. Ndivyo alivyofanya Ayubu sikuzote.


Naam, wewe wapuuza hofu ya Mungu, Nawe wazuia ibada mbele za Mungu.


Lakini ningewatia nguvu kwa kinywa changu, Na maliwazo ya midomo yangu yangewatuliza.


Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.


Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.


Kumtumaini asiye mwaminifu wakati wa taabu Ni kama jino lililovunjika, au mguu ulioteguka.


BWANA wa majeshi amesema hivi, ya kwamba, Fanyeni hukumu za kweli, kila mtu na amwonee ndugu yake rehema na huruma;


Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?


Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao.


Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.


Ni nani aliye dhaifu, nisiwe dhaifu nami? Ni nani aliyekwazwa nami nisichukiwe?


Mchukuliane mizigo na hivyo kuitimiza sheria ya Kristo.


Wakumbukeni hao waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao; na hao wanaodhulumiwa, kwa vile ninyi nanyi mlivyo katika mwili.